Jumanne, 7 Februari 2017

PERA



     Ni wakati mwingine ndugu mpenzi mfuatiliaji wa makala haya tunakutana tena kuelekezana kuhusu faida za lishe ya matunda mbalimbali.Leo tutaangalia umuhimu wa tunda la aina ya pera kwani wengi wamekua wakiniuliza kuhusiana na faida za tunda hili hata kabla sijachukua maamuzi ya kuliandika na kulitolea ufafanuzi
 Kwanza tuanze kumshukuru mungu kwa yote aliyotutendea na kutufikisha hapa tulipo kwa siku ya leo,kama ni mgonjwa unapaswa kumshukuru mungu pia na kutafuta njia gani ufanye ili uondokane na ugonjwa huo.Twende pamoja katika kuangalia faioda mbali mbali za tunda hili;

 Kama tunavyolifahamu tunda la pera ni tunda ambalo watu wengi hawapendi kulila kawaida kwani lina mbbegu ambazo ni ngumu sana ambazo hata watoto wadogo hawawezi kuhimili kuzitafuna.Kuna pera la kijani,njano na jekundu yote haya ni sahihi kuliwa lakini yanaonyesha hatua za ukomavu wake,lakini kwa pera la kijani mara nyingi huwa linakua bado bichi hivyo ukila pera hilo utasumbuliwa na tumbo kwani virutubisha vyake huwa bado havijakamilika.
     Licha ya kuwa na sifa hiyo hakumaanishi eti usle kabisa tunda hili hapana,unaweza ukalisaga na kutengeneza juisi ambayo itakufanya upate virutubisho vile vile ambavyo ungevipata kwa kulila likiwa lenyewe.Pera kama yaaalivyo matunda meeengine lina faida mbali mbali kama vile;

VITAMINI C
 Tumeona tangia mwanzo faida za vitamini C kwenye mwili wa binadamu na kama utakumbuka vizuri ni karibia kila aina ya tunda lina kirutubisho hiki hivyo kwa ujumla tunaweza kusema kwamba matunda ni chanzo kikubwa cha vitamini C.Kazi kubwa ya kirutubisho hiki ni pamoja na kuzuia magonjwa ya fizi na taya (Kiseyeye) hasahasa kwa watoto wadogo.Mpe mwanao kirutubisho hiki kwa kumkinga dhidi ya ugonjwa huu.Tunda la pera lina 120mg za vitamini C ambayo kwa mwanaume ni 90mg huhitajika kila siku na 75mg ambazo huhitajika kwa mwanamke.Faida nyingine ya kirutubisho hiki ni pamoja na kusaidia katika utengenezaji wa tishu mpya mwilini na kuchochea ufyonzaji wa chakula kilicho sagwa vyema mwilini,kwa kutokula pera na kukosa vitu hivi utaona ni kwa kiasi gani unakosa vitu muhimu.

MATATIZO YA UZAZI KWA WANAWAKE.
 Kuna kirutubisho kimoja aina ya FOLATE ambacho hupatikana ndani ya tunda hili la pera kinachofanya mayai ya mwanamke kukua vyema.Licha ya kuwa na tatizo la homoni za uzazi mwilini mwa mwanamke,anaweza kukabiliana na tatizo hilo kwa kutumia tunda la pera kama dawa ya tatizo lake na matokeo atayapata.Kwa dada mwenye matatizo ya uzazi kama kushindwa kuona siku zake na hata yule anayeshindwa kubeba mimba,kuna siri kubwa imefichika katika matumizi ya matunda siyo pera tuu bali hata na matunda mengine.kirutubisho hicho kina kazi nyingi zihusianazo na uzazi hivyo unaombwa kutumia tunda hilo kwaajili ya kuondokana na matatizo yasiyo ya lazima.

HUPUMZISHA MWILI.
 Uwepo wa vitamini B3 na B6 kunafanya mwili kuwa mtulivu na wenye mwendokasi uliotulia zaidi.Nakushauri baada ya kazi na uchovu wa mwili kula pera kwa ajili ya kuuburudisha mwili na kukufanya utulie kwa utulivu sahihi.Watafiti wanadai kuwa pera huuupa ubongo afya njema na mtulizo wa akili ulio sahihi na kuwa kufanya hivi huongeza uwezo wa utendaji kazi wa akili ya mtu,ukimwanzishia mwanao leo hii lishe sahihi ya tunda hili utamfanya kuwa na akili njema na ukuaji wake utasawijika kwani ni ubongo huo huo unaoooooorekebisha masuala ya ukuaji.

MATATIZO YA CHOO.
 Kamba lishe zilizopo ndani ya tunda hili zina mchango mkubwa sana katika kurekebisha matatizo ya choo,kwa wale wote wanaopata choo kigumu wanaweza wakaanza kutumia mapera kama njia mbadala ya kutibu tatizo lao.Pia kama una kumbukumbu nzuri utaona kwenye kila aina ya tunda tuliloliona mwanzo lina mchango mkubwa sana wa suala kama hili hivyo yunaweza kusema kwamba matunda yanatusaidia sana kukabiliana na tatizo hili.Kazi kubwa ya kambalishe hizi ni kusaidia usagaji wa chakula mwilini na ufyonzwaji wa maji katika sehemu ya mwisho ya usagaji yaani kwenye utumbo mkubwa.

DAWA YA TUMBO.
 Hapa ifahamike wazi kwamba majani ya mti wa mpera yana mchango mkubwa sana katika kutibu tumbo lolote lile liwe la kuhara au kuuma kwa kawaida.Sio dawa yenye masharti wala haikuhitaji kulipia hata gharama zaidi ya muda wako tuu,unashauriwa kuchukua majani machanga ya mpera na unaweza ukayatafuna bada ya kuyaosha au ukayachemsha kwa muda wa dakika kumi na ukanywa maji yake hayo kwa kipimo sahihi (usisubiri yapoe).

MZUNGUKO WA DAMU.
 Kutokana na kiasi kikubwa cha madini ya mangenese na iron iliyopo ndani ya tunda hili ni mchango mkubwa katika utengenezaji wa damu kwani madini ya chuma ndiyo hasa yanahitajika kwaajili ya kutengeneza damu.Uwepo wa madini haya mwilini kutokana na ulaji wa mapera utakuwezesha kukufanya uwe na utajiri mwingi wa damu na kuondoa matatizo yote yatokanayo na upungufu wa damu.
Pera pia lina kiasi kikubwa sana cha FOLIC acid ambayo ndiyo hitaji kuu la utengenezwaji wa damu ukitilia ndani madini ya iron.Asidi hii husaidia kuzuia ugonjwa wa anaemia kwani ndio ugonjwa mmojawapo utokanao na uchache wa damu mwilini.

  Antioxidant (kiondoa sumu) kilichomo ndani ya pera kina kazi muhimu san aya kutibu na kuondoa bacteria wasiohitajika tumboni,baadhi ya bacteria waliopo tumboni huzaliana kwa wingi na kusababisha hata UTI kwa wanawake.Si hayo tuu bali na magonjwa mengi kama kichwa kuuma,miguu na hata kuhara pia huondolewa kwa ulaji wa tunda hili,chukua maamuzi sahihi kama unaijali afya yako sasa.
   Anza sasa na usisubiri kwa ni bado hujachelewa,fuata kanuni sahihi za lishe ili kuondokana na magonjwa yasiyo ya lazima uwe na afya bora.
Kwa maelezo,maswali na ushauri kuhusiana na afya yako usisite kuwasiliana nasi kwani tupo kwaajili ya kukufahamisha na kuhakikisha tuna share kile tunachokijua nawe pia ufaidike...Ahsante

PHONE: 0673666791

Email: goldamplat@gmail.com

Ijumaa, 3 Februari 2017

APPLE (TUFAA)

    Habari za muda huu ndugu mfuatiliaji wa makala haya,ni matumaini yangu u mzima wa afya na kama una matatizo ya kiafya,kiroho na hata mengine yatofautianayo na hayo ni wakati wako kumgeukia mungu na kumuomba akupe njia ya kuweza kukabiliana nayo.

Leo nimewiwa kukuletea matumizi sahii ya matunda katika afya zetu dhidi ya kujikinga na kupambana na magonjwa mbalimbali na tutaangalia umuhimu wa tunda aina ya apple (tufaa).Je unakumbuka ile kauli ya APPLE EATING KEEPS AWAY FROM DOCTOR? Basi kama hukumbuki basi ndivyo ilivyo na ni kweli kutokana na kazi nzuri zifanywazo nz tunda hili.

    Matufaa yana Vitamini K,nyuzinyuzi za chakula pamoja na dawa-lishe (phytochemicals) aina ya quercetin flavonoid hivyo kukuwezesha kupata virutubisho sahihi vinavyohitajika na mwili wako.matatizo mengi huondolewa na tunda hili na kukufanya uwe na mwili mwepesi pamoja ana afya njema kama utafuata taratibu za lishe katika matunda haya.Tuangalie faida zake kiafya;

HUREKEBISHA AFYA YA MAPAFU.
 Katika matunda ambayo yana mchango mkubwa juu ya magonjwa na matatizo ya mapafu ni pamoja na tunda hili,umaarufu wake umetokana na kazi kubwa ya kurekebisha maswala ya mapafu.Majimaji yaliyopo kwenye apple yana mchango mkubwa sana juu ya kuondoa bakteria ambao wanavamia mapafu na kuleta magonjwa kama kifua kikavu.
Kuna asilimia kubwa kwa apple kutibu kansa ya mapafu kutokana na kazi za kuzuia maambukizi ndani ya mapafu,wataalamu wengi wameshauri kula tunda hili kwa lengo la kurekebisha afya yako ya mwili mzima kiujumla.

HUZUIA MAWE KWENYE FIGO.
 Kwa kurekebisha mzungoko mzuri wa damu mwilini,apple linauwezo mkubwa wa kusafisha damu yako na kufanya ini pampja na figo kupunguziwa kazi ya kuchuja taka mwili ndani ya mwili.Magonjwa ya ini na figo huzuiliwa kwa tunda hili la apple.

SOLIDI YA TUMBO (COLITIS).
 Kama unasumbuliwa na tumbo la kuhara na hujisikii vizurim kila baada ya kula unashauriwa kuanza mara moja kutumia tunda hili kama kinga kwani linasaidia katika kurekebisha udhaifu wowote wa tumbo.
Ulaji wa apple unatia nguvu mwili na kukufanya kukaa muda mrefu bila kusika njaa au uchovu.Ma apple matatu yanakufanya kukaa masaa nane pasipo kuhisi uchovu mwilini mwako na kukuweka active kwa muda wote huo.

MAGONJWA YA KUHARISHA.
 Hii huonekana katika mambo yote mawili kwenye kuharisha au kupata choo kigumu nyuzi nyuzi zilizopo ndani ya tunda hili kama kwenye matunda mengine tuliyoyaona hapo awali,zitakufanya uondokane na tatizo kama hili.
Tumia kwa lengo la afya na sio kwa mazoea kama kusitisha matumizi au kula ukijisikia kufanya hivyo kwani hutaona manufaa yoyote na utaishia kulalamika kwamba hujapata matokeo mazuri.

MATATIZO YA DAMU.
 Matatizo kama blood pressure na anaemia hurekebishwa kwa ulaji wa matunda haya kwani lina kiwangi kikubwa cha calcium 10mg ambacho huweka sawa uwiano wa minerals zipatikanazo ndani ya damu.hupunguza kiasi cha Nacl ambacho hutofautisha na kufanya pressure ipande kwa kiasi kikubwa katika damu na kurudisha uwiano sawa 
 Kwa uwingi wa iron na arsenic pamoja na phosphorus husaidia kuongeza madini muhimu katika kurekebisha damu yako mwilini.

NB: Ulaji wa apple moja kwa siku ni zaidi ya mtu aliyekula mikate mitano isiyotiwa amira.

  Ulaji wa matunda haya kila siku utakufanya umsahau daktari na kukuweka mbali na hospitali,pia utamsababishia daktari kukosa ajira yake.
Nakushauri kuanza leo kutmia tiba hizi ili iwepo tofauti kati yako wewe na mtu ambaye alipuuzia ili apate mfano kwako jinsi ya afya yako itakavyokua bora.
Usisite kuwasiliana nasi muda na saa yoyote kama uan swali au maoni yoyote kuhusiana na afya yako...Ahsante

PHONE:  0673666791

Email: goldamplat@gmail.com

Jumatano, 1 Februari 2017

ZAITUNI.


   U hali gani ndugu msomaji wa makala haya ya AFYA KWANZA,ni matumaini yangu uko poa na mwenye afya njema tunapaswa kwa pamoja kumshukuru mungu kwa kutufanikishia jambo hilo.

     Leo tena ni siku nyingine ambayo tutaeleweshana kuhusu mambo fulani yahusuyo afya zetu kutokana na ulaji wa tunda aina ya zaituni.Tunda hili linaweza lisijulikane na wengi miongoni mwetu kwani linaoatikana kwa asilimia ndogo nchini ketu lakini limeonekana kuwa na kazi nyingi muhimu katika miili yetu.Tuangalie baadhi ya kazi zake hizo ni kama ifuatavyo:

HUPUNGUZA UZITO
 Tunda la zaituni limekua likiorodheshwa sana kwenye lishe za kupunguza uzito/unene,hii ni kutokana na ukweli kwamba tunda hili lina mafuta (olive oil) mepesi ambayo hayawezi kuganda ndani ya mwili na matumizi yake hutumika haraka baada ya kuonekana ndani ya mwili.Kwa watu wenye uzito uliopitiliza niwashauri kuanza kutumia tunda hili.

KUONGEZA NGUVU ZA KIUME.
 Kutokana na kurekebisha afya ya damu mwilini na kukupa nguvu ya mzunguko mpya mwilini,hamu na uwezo wa kimapenzi huongezeka ndani ya mwili wa mtumiaji wa tunda hili.Kutokana na uwezo huo watu wamekua wakilisifia tunda hilo kwa kazi yake hiyo kubwa bila kujua linafanya nini kukamilisha kazi hiyo.

TATIZO LA MAFUA.
 Wengine hutumia mafuta ya mizeituni (olive oil) kupaka kwenye upeo wa eneo la mbele ya pua kama dawa ya kutibu ugonjwa wa mafua,lakini mpaka sasa bado haijafahamika wazi ni kwanini mafuta haya hutibu mafua kwa dizaini kama hiyo ya VIKS-KINGO.

MAGONJWA YA NGOZI.
Hii ni kweli na inasaidia kwa kiasi kikubwa sana kwa mtumiaji kwani tunda la zaituni lina kiwango kikubwa sana cha vitamin D ambayo ndiyo hasa hutumika katika kurekebisha matatizo ya ngozi.Paka mafuta ya mizeituni na utaona tofauti ndani ya muda mchache

HUREKEBISHA TATIZO LA NYWELE.
 Kwa wale wenye nywele za kukatika na zilizojikunja,unaweza kutumia mafuta haya kwa kuzirefusha na kuzuia zisijikunje tena,vitamini D iliyopo ndani ya tunda hili husaidia kwa kiasi kikubwa kurekebisha afya ya ngozi kwenye kichwa ambayo huruhusu ukuaji mzuri wa mizizi ya nywele.Unaweza kuona wazi kwamba mafuta mazuri ya nywele ni OLIVE OIL.
            NB: Isionekane kama nafanya promotion ya baadhi ya mafuta ya nywele na vipodozi,Hapana.

HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KANSA
Mafuta ya zeituni (olive oil) yana olecanthal na of mimics inayozalisha ibuprofen inayosaidia  kupunguza hatari ya kupata cancer.Ni mafuta mazuri kwa yule atakaye jali afya ya mwili wake na kuitetea na ifahamike wazi kwamba wapo wagonjwa wa kansa ambao wanatumia mafuta ya mizeituni katika mlo wao wa kila siku kama kupunguza /kufisha sumu ya kansa mwilini.

NI DAWA SAHIHI YA UBONGO.
 Hii ni kwa watoto wadogo ambao wanakua,virutubisho vipatikanavyo kwenye mafuta ya tunda hili likiwa bado halijapikwa ni muhimu sana ukilinganisha na vile ambavyo hupatikana baada ya kuyapika mafuta hayo.Muanzishie mwanao utaratibu wa kumnywesha mafuta mabichi ya mzeituni ili kulinda afya yake na kumfanya awe mchangamfu na mwenye akili timamu.

DAWA YA MASIKIO KWA WATOTO WADOGO.
 Watoto wenye matatizo ya masikio kama kuwashwa mara kwa mara na kutokwa na uchafu mwingi mwilini wnaweza wakaondokana na tatizo hilo kwa kumuanzishia dozi ya mafuta hayo.Matone mawili mpaka matatu mara mbili kwa siku kutafanya tatizo hili kupotea kabisa.
Ifahamike wazi kwamba mafuta ya mzeituni (olive-oil) baada ya kupikwa hupoteza ubora wake na kutengeneza sumu lishe ambazo zitatolewa nje ya mwili bila kufanya kazi yoyote.Hivyo basi ni muhimu kuanzisha utaratibu wa kutumia mafuta mabichi ya mizeituni kuliko kuya[pika kwanza.

Kwa ushauri na maswali kuhusiana na tatizo lolote linanalo kusibu,usisite kuwasiliana nasi kwa namba hizo apo chini,,,,,Ahsante.

         Pia kuna matumizi ya kiimani kuhusiana na mafuta yatokanayo na matunda haya.
    NB: Ikumbukwe kwamba hatutolei mafunzo ya afya kwanza kutokana na imani ya mtu fulani,bali hata wasioamini nao wana haki katika jamii inayowazunguka.

                       PHONE:  0624259822

Jumatatu, 30 Januari 2017

  UKWAJU.


    Habari ndugu mpenzi msomaji wa makala haya,nakukaribisha tena ili kufahamu umuhimu wa tunda lingine aina ya Ukwaju.Ni tunda la tofauti kidogo kati ya matunda mengine ambayo tumekwisha yaona hapo awali lakini leo ngoja tuangalie umuhimu wa utofauti wake na matunda mengine.

    Kidogo ni tunda la kushangaza kwani lina ladha tamu na chachu,tunda hili unapoanza kula kwanza lazima likusisimue ndipo uendano nalo na imekua ni vigumu kwa watoto wadogo kulila tunda hili wenyewe kama wenyewe kutokana na ladha yake.Ulaji wake haujatofautiana na matunda mengine kwani unaweza kulila kama tunda,ukatengeneza juisi na ukanywa na hata ukatumia kama siagi.Kusema kweli ni tunda lenye maana kubwa kutokana na kazi lilizokua nalo,tuangalie baadhi ya kazi hizo ni kama ifuatavyo.

HUTIBU HOMA.
 Kuanzia homa ya tumbo mpaka homa ya manjano tunda hili hutibu pasipo kuangalia.Hii ni kutokana na asidi liyopo ndani ya tunda hili inayozuia kabisa uzalianaji wa bacteria hatari ndani ya tumbo na kuwaacha wale wanaohitajika kubaki tuu.Imetumika kama dawa yenye manufaa zaidi kwani mtu akiumwa tumbo na kutumia ukwaju basi amejihakikishia pona yake.

HUSAIDIA USAGAJI WA CHAKULA.
 Kama yalivyo matunda mengine,ukwaju una nyuzi nyuzi ambazo husaidia katika usagaji wa chakula na kukupa choo kizuri kama tulivyoona katika matoleo ya nyuma.Kwa mwenye tatizo kama hili hatakiwi kuuliza afanye nini ili aweze kujiponya wakati dawa ya ukwaju tayari ipo na inapatikana sokoni.

HUTIBU VIDONDA.
 Vidonda vya kuungua hupona kwa kutumia ukwaju,lakini mara nyingi hutokana baada ya mchanganyiko wa tunda hili na asali.Mchanganyo utakaotumika kama dawa unatofautiana kulingana na sehemu ya jeraha au ukubwa wa jeraha pia.

HUTIBU MAAMBUKIZI YA KOO.
 Bakteria pamoja na protozoa wengine wanaoshambulia mfumo wa upumuaji huzuiwa kufanya hivyo mara tuu wanapotaka kuingia kwenye sehemu za ndani kabisa za mfumo huo kutokana na asidi inaypatikana ndani ya tunda hili,hii itakuweka huru na magonjwa yote ya koo na hata ya mfumo wa chakula kwani ni koo hilohilo ndilo linalounganisha mifumo hiyo miwili.

HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KANSA.
 Tunda la ukwaju limewasaidia wengi katika kurekebisha afya zao na kupunguza uwezekano mkubwa wa kupata kansa kwani ladha yake ya uchachu hairuhusu ukuaji wa kansa mwilini.Unashauriwa kutumia mara kwa mara ili kupunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kupata kansa mwilini mwako.Kinga za ukwaju zitazuia ukuaji wa kansa kama zitapatikana kwa wingi mwilini mwako na si vinginevyo.

UKOSEFU WA HAMU YA KULA.
 Kwa wale wanaokosa hamu ya kula chakula,tunda la ukwaju ni msaada mzuri kukurejesha katika hali yako madhubuti.Ingawa watoto wengi hukumbwa na tatizo hili pale ambapo wanakua au wamepatwa na homa,andaa juisi yako ya ukwaju na kisha tumia kikombe kimoja nusu saa kabla ya kula utaona mafanikio.

    kutokana na kazi hizo,tunashauri tunda la ukwaju lisikose katika mlo wako wa kila siku kwani lin kazi kubwa sana ukilinganisha na matunda mengine ingawa baadhi zinafanana.Tumia ukwaju kama dawa kama ninavyokwambia kwenye matunda mengine na sio utumie pale ambapo unaona tatizo limekufika kwani hata kama utapata mafanikio hayatakua makubwa kwani matunda mengi ni kinga dhidi ya magonjwa na machache ni dawa hivyo unapaswa kutumia kwa kujitaadharisha na magonjwa yajayo.

  Kama utakua unafanya hivyo kwa utaratibu wa kujiwekea ulinzi na akiba ya kinga mwilini utakua mbali kiafya na hautasumbuliwa na magonjwa nyemelezi kirahisi,lakini hakikisha unamshauri na ndugu au rafiki na hata mwenzako uliye nae jirani kufuata kanuni na taratibu za afya ili aepukane na magonjwa.
  Sina la ziada kwa siku ya leo,kwa maswali juu ya afya yako na ushauri wowote usisite kuwasiliana nasi tutakusaidia vyema kwa wakati wowote na muda wowote.Ahsante

Kwa mawasiliano usisite kututafuta;

  PHONE : 0673666791

  Email:  goldamplat@gmail.com

Alhamisi, 26 Januari 2017

ZABIBU.




     Ni matumaini yangu u mzima wa afya na unaendelea na majukumu yako ya kila siku katika kujenga nchi yenye nguvu.Nchi imara haiwezi kuja kama wajenzi wake wana afya dhaifu itakua ni dhahania hivyo hakikisha unafuata kanuni za mlo wa afya na kinga mwilini mwako ili kupata afya iliyo thabiti.
  Leo mezani kwangu nimekuandalia tunda lingine ambalo ni moja kati ya tunda la karne na karne lenye sifa na uwezo mkubwa,nalo si lingine bali ni Zabibu.

  Katika matunda yaliyojizolea umaarufu mkubwa kuanzia karne ya sita ni tunda hili.ni la zamani sana na lilitumika kutengenezea pombe (mvinyo) tangu enzi za watu wa kale.Kusema ukweli tunda hili ni tamu na linapendwa na kila mtu hasa hasa na watoto.
  Kuna aina tatu ya zabibu nayo ni zabibu za kijani,nyekundu na kama nyeusi (dark-red),aina zote hizi huliwa kwa njia mbalimbali kama vile kwa kutengenezewa juisi,zabibu zilizo kaushwa kama raisin na kama tunda la kawaida  kama matunda mengine.Tuangalie faida kuu za tunda hili;

 VITAMINI B COMPLEX.
  Karibu aina zote za vitamini B unazozifahamu zipo humu kwenye zabibu,hii inalipa sifa tunda hili kurekebisha matatizo yote yarekebishwayo na vitamini hizi.Kuna kama vile magonjwa ya damu na mengineyo.

HUTIBU PUMU.
Tunda hili lina maji kiasi chacke ambayo kazi kubwa ni kuongeza unyevunyevu ndani ya mapafu na kupunguza uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa unaohusiana na njia hiyo ya hewa.Dawa nyingi za mitishamba ambazo hutumika kutibu pumu huchanganywa na unga wa zabibu zilizo sagwa na kukaushwa vizuri.

HUONDOA SUMU.
Viondoa sumu (anti-oxidants) ambavyo hupatikana kwenye tunda hili vina kazi kubwa sana kuachilia mbali nguvu inayotolewa kwenye maziwa.Mgonjwa ambaye amekunywa sumu mara tu na hakuna uwezekano wa maziwa jirani,unaweza kumpa juisi ya zabibu kama ipo jirani na hii itamsaidia.

HEREKEBISHA TATIZO LA DAMU.
Zabibu huongeza kiwango cha nitric acid mwilini ambacho huzuia damu kuganda.pia inaaminika kwamba juisi ya tunda hili inaongeza damu kwa mtumiaji anayeitumia mara kwa mara na husaidia kupunguza tatizo la moyo linalosababishwa na damu kuwa chache mwilini

HULAINISHA CHOO.
ukweli ni kwamba zabibu lina kiasi cha kawaida cha kamba lishe ambacho hufanya kazi ya kurekebisha choo kikubwa.Watoto wengi wanaokosa maji mwilini kutokana na wazazi kushindwa kuwapa maji ya kutosha,wanaweza kuanzishiwa utumiaji wa juisi ya tunda hili.

HUPUNGUZA MAFUTA MWILINI.
 Zabibu halina mafuta,hii husaidia kurekebisha uwingi wa mafuta yaliyomo ndani ya mwili kwani yana kiwango kikubwa cha carlories ambazo hushawishi matumizi ya mafuta kwa kuzalisha nguvu mwilini pindi ambapo zimekwisha carlories hizo.
  Tunda hili ni tamu na huweza kuliwa kwa kupitiliza kutokana na ladha yake,kumbuka kwa kufanya hivyo huendani na kanuni za afya bali unajiongezea uchafu mwilini kwani kiasi kidogo kinachohitajika kitachukuliwa na kilichobakia kitatolewa nje kama makapi ."Kula kwa afya na sio ule kwa kuwa kipo" nakumbuka zamani mama alikua anapenda sana kutumia maneno hayo akimaanisha nile kwa kiasi.

  Hata mimi leo sina budi kukushauri kwa matokeo thabiti ya afya yako tumia kiasi kidogo mara kwa mara kama ulivyoelekezwa hapo juu na hakika matokeo yake utayapata ndani ya muda mfupi.
Kwa ushauri,maoni au maswali kuhusiana na matatizo ya kiafya usisite kuwasiliana nasi kwa mawasiliano hapo chini....Ahsante.

PHONE;  0673666791

Email; goldamplat@gmail.com 

Jumatano, 25 Januari 2017

KAROTI.


          Habari ndugu mpenzi msomaji wa makala haya,nakukaribisha tena ili kufahamu umuhimu wa tunda lingine aina ya Karoti.Ni tunda la tofauti kidogo kati ya matunda mengine ambayo tumekwisha yaona hapo awali lakini leo ngoja tuangalie umuhimu wa utofauti wake na matunda mengine.
   Kwanza hili ni tunda pekee ambalo linaweza kupikwa na lisiharibu ladha yake,pia linaweza kuliwa likiwa kama matunda mengine yanavyoliwa bila kupikwa.Pia tunda hili ni moja wapo kati ya matunda machache ambayo yanaoatikana chini ya ardhi,tumezoea matunda mengi hupatikana juu ya miti au hata yakiwa yamelala ardhini lakini sio chini ya ardhi kwa kufanya kuyafukua/kuchimba.

  Kuna aina tatu za karoti ambazo hutofautiana kwa rangi zake,kuna karoti nyekundu,ya njano na ya pinki lakini zote ni karoti.Karoti za njano na nyekundu ndizo zenye virutubisho vingi ukilinganisha na hiyo ya pink na mara nyingi ndizo aina za karoti ambazo hulimwa sana nchini kwetu Tz.
    Karoti kama yalivyo matunda mengine lina faida kubwa sana nyingi,watu wengi tumekua tukisikia faida moja tuu ya kutibu macho na kuyafanya yawe maangavu.Ni kweli lakini siyo kazi hiyo tuu bali kuna kazi nyingi za aina mbalimbali,ungana nami tuzione hapo chini;

 HUTIBU MATATIZO YA CHOO.
  Karoti lina kiasi kikubwa cha kamba lishe ambazo ndizo muhimu katika kurekebisha tumbo na kukupatia choo kizuri.Kambalishe hizi husaidia katika ufyonzaji wa maji katika njia ya mwisho ya usagaji wa chakula hivyo kukuweka katika hali nzuri kama zitapatikana kwa kiasi kikubwa mwilini.

 HULAINISHA NGOZI.
  Kwa mtumiaji wa karoti mara kwa mara atakubaliana na mimi kwa kazi hii ambayo karoti inafanya,warembo wengi wanatumia mafuta na losheni za ngozi zilizotengenezwa na tunda hili kwaajili ya umakini wa ngozi zao.Hii inatokana na uwepo wa vitamini E iliyopo ndani ya karoti inayofanya kazi ya kurudisha na kutengeneza seli mpya za ngozi zilizo haribika/kufa.

 HUFANYA MACHO KUWA MAANGAVU.
  Karoti ina kirutubisho kiitwacho Beta-carotenene ambacho ndio chanzo muhimu cha vitamini A mwilini.Baada ya kubadilishwa na kuwa vitamini A mwilini,carotenene hupelekwa moja kwa moja katika utengenezaji wa seli ndani ya pupil na retina kwenye macho.Hii hufanya uwingi wa seli hizi na kusababisha kuondoa tatizo la kutokuona kwenye mwanga hafifu au mdogo.

 HUONDOA TATIZO LA CHUNUSI.
  Kama tulivyoona hapo juu vitamin E ndiyo hasa itumikayo kupambana na magonjwa ya ngozi,hivyo kwa uwepo wa vitamini hii hutatua tatizo la chunusi na vipele vitokanavyo na mafuta mengi usoni.

CHANZO CHA NISHATI MWILINI.
 Karoti haina mafuta bali ina karolies nyingi,hivyo kwa mtumiaji wa karati hupata virutubisho hivi kwa wingi na kumfanya awe na nguvu za kumwezesha kuhimili kazi mbalimbali.

 HUREKEBISHA TATIZO LA DAMU.
  Juisi ya karoti inasifika kurekebisha tatizo la upungufu wa damu mwilini,kwa matumizi ya kama dawa unashauriwa kutumia ndani ya muda wa si chini ya miezi mitatu.Kunywa glasi moja ya juisi kila siku kwa matatizo ya damu.

  Karoti ni muhimu sana kwa watoto wadogo kwani ina vitamini A nyingi ambazo zitamjengea mtoto kinga nzuri juu ya magonjwa mengine mengi tofauti na ya macho.Unashauriwa kumwanzishia mtoto wako mdogo utaratibu wa kunywa juisi ya karoti kama dawa kwa kumkinga na monjwa mengine mengi.
Tunda hili limekuwa na sifa nyingi kutokana na kazi yake kubwa moja ya kutibu macho.
   Kwa kuwa na viondoa sumu vingi ndani ya karoti,imekuwa na mchango mkubwa wa kutibu magonjwa ya kansa kama vile kansa ya mapafu,tumbo na tezi za uzazi za kiume.
Kwa faida nyingine nyingi tazama; http://www.a2ztube.co.
  Kwa lolote linakusumbua kuhusu afya yako usisite kuwasiliana nasi kwa ushauri na kukujibu maswali yako.Pia tunatoa huduma za kufundisha taratibu za milo mingine kwa ajili ya matatizo ya afya yatokanayo na mfumo wa maisha...Ahsante.

PHONE;  0673666791

Email: goldamplat@gmail.com

Jumapili, 22 Januari 2017

 TIKITI-MAJI.



     Leo tena katika makala nyingine tunakutana kuzungumzia tunda aina ya Tikiti-maji,kabla ya kuanza mada yetu hatuna budi kumshukuru Mungu kwa yote aliyotutendea na kutuweka salama mpaka muda huu.Ni matumaini yangu ni wazima wa afya na mmejaaliwa kuiona siku nyingine hivyo sifa na utukufu arudishiwe Mungu muweza yote.

  Kama wengi jinsi tunavyolifahamu tunda hili kuwa na uwingi wa 92% ya maji pekee ndivyo kazi yake kubwa yakuhakikisha maji mwilini mwa mtumiaji hayapungui.Tikiti-maji lina aina mbalimbalio za madini ambayo hufanya kazi nyingi mwilini mwetu na kusaidia kuboresha afya ya mlaji.
Tuangalie baadhi ya kazi muhimu za tunda hili;

HUONGEZA NGUVU ZA KIUME.
 Kila kipatikanacho ndani ya tunda hili kina kazi kubwa ukianzia majani,maganda pamoja na mbegu.Wanaume wengi wamekua wakikumbwa na tatizo la hili na kumekuwa na matangazo mbalimbali kuhusiana na dawa za kusaidia tatizo hili.Ndugu msomaji ni bora kutumia dawa za matunda/lishe ili kutibu au kupunguza au kuzuia tatizo lako na sio kila dawa kuiona inafaa.Mbegu za tunda hili zikiliwa pamoja na nyama ya tunda hili husaidia katika kurekebisha upungufu wa nguvu za kiume kwa asilimia kubwa kuliko inavyotegemewa.Watu wengi wamejaribu kufanya hivyo na matokeo wamerudisha sifa na shukrani kwa somo hilo,tuwasiliane kwa maelezo zaidi.

HUONDOA SUMU MWILINI.
  Lycopene ipatikanayo ndani ya tunda hili husaidia kuzuia sumu mbalimbali mwilini zisiudhuru.Pia sumu zipatikanazo kwenye baadhi ya nyama (protini) hurekebishwa kwa kirutubisho hiki.Pia baadhi ya protini ngumu tunazokula kila siku husagwa nakufanywa nyepesi kuchukuliwa ndani ya mwili na kufanya kazi husika kuliko kutolewa nje kama uchafu/kinyesi.

HUSAIDIA MATATIZO YA CHOO NA UPUNGUFU WA MAJI.
 Kuwepo kwa maji kwa asilimia nyingi pamoja na kamba lishe,kunasaidia kurekebisha matatizo ya choo na kibofu cha mkojo.Kwa wenye magonjwa haya,kwa kutumia tunda la Tikiti-maji wataweza kuyatibu na kuyazuia na kwa wale ambao hawana wanashauriwa kutumia tund hili ili kujihakikishia ulinzi wa afya zao na wasisubiri mpaka wakutane nayo.

HUPUNGUZA SHINIKIZO LA DAMU KWA KIWANGO KIKUBWA.
 Utafiti uliofanywa na watu wamarekani ulibaini kuwa watu wengi walio na tatizo la shinikizo la damu (PRESURE) na wakatumia tunda hili katika milo yao waliweza kupunguza kasi ya tatizo hilo.
Hii inatokana na uwepo wa sukari asilia ambayo ni muhimu kurekebisha kiwango cha sukari mwilini na kukuleta kiwango sawa cha sukari inayohitajika.

MAGONJWA YA MENO NA MIFUPA. 
  Tikiti-maji lina madini kama vitamini C ambayo husaidia kuzuia magonjwa ya fizi pamoja na meno (KISEYEYE),hivyo ulaji wa tunda hili hasa kwa watoto utapunguza kasi ya athari za ugonjwa huu.
Watoto wengi pia hulipenda kutokana na sukari yake iliyomo ndani ya tunda hili hivyo haitakua vigumu mtoto kulila kwani kuna baadhi ya matunda ambayo sio rafiki kwa watoto na asilimia kubwa hayapendwi kutokana na uchachu,uchungu au kiwango kidogo cha sukari kinachopatikana.

HUIMARISHA UBONGO.
 Uwepo wa vitamini Bcomplex (B6) kwenye tunda hili husaidia kuimarisha kazi ya ubongo na kuufanya kuwa mchangamfu kwa muda mrefu.Baadhi ya matatizo yanayoyaukumba ubongo huweza kuzuiwa na kurekebishwa na vitamini hiyo.Unashauriwa kama wewe ni mwanafunzi utumie tunda hili kwa manufaa ya kuufanya ubongo wako kuwa active.Vilevile hata kwa wazee na walevi wanaokutana na matatizo ya kusahau watakuwa vizuri endapo watatumia tunda hili.Si kuimarisha tuu bali tunda hili hutumika kama lishe ya ubongo.


   Siyo ivyo tuu,licha ya kuchangia kwa kiasi kikubwa urekebishaji wa tatizo hilo tunda hili lina uwezo mkubwa sana wa kusaidia moyo kuweza kufanya kazi kwa kiwango sahihi na sio kuzidiwa na kazi.Hii husababisha kuupa moyo muda wa kutosha wa kupumzika kwa kufanya kazi kidogo.
  Unaweza aukatumia tunda hili kama juisi na pia ukala kama unavyokula matunda mengine ila vyote hufikisha virutubisho mwilini,lakini pia kwa matatizo mengine ambayo tumeyaona hapo juu unashauriwa kutengeneza juisi ya tunda hili bila kuondoa kitu chochote kile nikimaanisha kuanzia maganda mpaka mbegu zake.
      Anza mazoea sasa yakutumia matunda kama lishe mbadala na kinga dhidi ya magonjwa na usisubiri mpaka ukutane na magonjwa ndipo ukumbuke kuna lishe ya matunda,fanya hivyo kwa manufaa ya afya yako binafsi na sio kwa kulazimishwa wala kuiga ulaji wa mtu mwingne.
Ifahamike wazi kwamba ulaji wa matunda kiafya haukusababishii wewe usimwone daktari,bali kuna matatizo mengine ambayo ni lazima ukafanyiwe uchunguzi na ukatibiwe kwa mtaalamu wa afya kwani yanaweza kuwa ni zaidi ya ufikiriavyo.
 Kwa maoni,ushauri na mengineyo usisite kuwasiliana nasi kwa mawasiliano hapo chini. Ahsante

PHONE:  0673666791

Email: goldamplat@gmail.com