Alhamisi, 16 Februari 2017

 Amplat AFYA KWANZA.

  Ni wasaha mwingine tena tunakutana katika kuelimishana juu ya umuhimu wa baadhi ya matunda kiafya,tuanze kwa kumshukuru Mungu kwani ndiye muweza wa yote na ametujalia kuwa wazima mpaka sasa.Natumaini tunaendelea na utaratibu wa kufuata lishe sahihi za matunda ilimkujikinga na magonjwa na kuziepusha hata familia zetu,Tujipongeze kwa hilo.

       Leo nakukumbusha umuhimu wa matumizi ya matunda kulingana na vitu vyote tulivyoviona tangu tulipoanza mpaka siku ya leo ili kama umesahau ukumbuke unapaswa kufanya nini na usijione kama upo peke yako.Nashukuru kwa wale wote tuliowasiliana nao nikawaeleza kulingana na walivyohitaji na sasa wananipa matokeo sahihi wakisema kwamba hawakujua mapema uwezo mkubwa wa matunda juu ya miili yao.Hakika si dhahania matunda yana nguvu kubwa sana katika kuijenga na kuilinda miili yetu kwa aina mbali mbali dhidi ya magonjwa nyemelezi.

    Kwa wewe ambaye umetumia kulingana na maelekezo na haujaona tofauti yoyote kabla na baada ya kutumia,nikukaribishe kwa kuchukua simu yako na kuwasiliana nasi kwa namba zetu hapo chini ili tukuelekeze zaidi nini cha ziada ufanye au kama ulikosea juu ya matumizi tukuifuatilie kwa ukaribu ili kukupa maelekezo sahihi juu ya afya yako.Nina imani kwa wale wote waliotilia nia na kushughulikia swala hilim wameona matokeo yakuridhisha kwani hakuna uongo wala siasa katika kutumia matunda kama lishe bora.Tunda la kulainisha ngozi (parachichi),litalainisha ngozi na tunda la kuondoa sumu (tango) litaondoa sumu na sio siasa,hivyo basi nikutoe hofun wewe ambaya umetumia dawa lishe ya matunda na haujaona tofauti.

  Amplat AFYA KWANZA ipo kwaajili ya kukupa elimu juu ya umuhimu wa lishe bora za matunda pamoja na kukusaidia katika kutatua matatizo yako kiafya kwa kukuunganisha na daktari unaestahili huduma zake kulingana na tatizo lako.Usiogope kuuliza pale usipoelewa ufanyaje ili upate lishe kamili ya utumiaji wa matunda sisi tupo kwaajili ya kutoa msaada.

   Ewe mama,dada,kaka,baba na watoto pia,kuwa na afya bora ni haki yako ya msingi hivyo nakushauri unapoona haupo sawa kiakili,kiafya na hata kimawazo usisite kuwasiliana nasi tutakusaidia.Kukaa kimya wakati una tatizo la afya sio vyema na waswahili husema kwamba MFICHA MARADHI KIFO HUMUUMBUA sasa basi usisubiri mpaka mauti ikufike ndipo tujue kwamba ulikua unaumwa nini.Mara tu uonapo hali ambayo si ya kawaida mwilini mwako usisite kutujulisha nasi tutakusaidia...Ahsante

PHONE:  0673666791

Email:     Goldamplat@gmail.com