Ijumaa, 6 Januari 2017

PARACHIHI.


Habari za muda na wakati mwingine tena ndugu msomaji,ni matumaini yangu u mzima wa afya na Mungu anakujalia katika mambo unayoyafanya kila siku hivyo huna budi kumshukuru.Katika kipindi kilichopita tuliona umuhimu wa tunda aina ya ndizi,na leo tutaangalia umuhimu wa tnda lingine aina ya parachihichi.
   Katika utafiti mmoja uliofanywa huko marekani ulionyesha kuwa watu wanaokula parachichi huwa na afya bora na wenye kunawili na kung"aa kwa ngozi zao ikilinganishwa na watu ambao hawatumii tunda hili.Kutokana utofauti na matunda mengine,parachichi linapendwa sana watoto wadogo kwani ni rahisi kulimeza.Hii inatokana na uwingi wa mafuta yapatikanayo ndani ya tunda hili ukilinganisha na matunda mengine yenye uwingi wa wanga pamoja na vitamini.tunda hili pia lina kiasi kikubwa sana cha madini ya aina ya potashium,fosforasi na magineziamu,bila kusahau vitamini zilizopo humu kama vile vitamini A,E na C.Tuangalie umuhimu wa parachichi kiafya.

    MAGONJWA YA MOYO NA SHINIKIZO LA DAMU.
Magonjwa ya moyo mara nyingi hutokana na mtindo wa maisha na vyakula tunavyokula kila siku,mafuta mengi tunayotumia huongeza kiasi kikubwa cha LEHAMU mwilini hupelekea kujirundika ndani ya mishipa ya damu na kusababisha presure za kupanda na kushuka.Kwakuwa parachchi lina mafuta mengi yasiyokua na lehamu,hivyo nibora litumike kama mbadala wa kupunguza mafuta yasiyohitajika mwilini.

    KUPUNGUZA UZITO WA MWILI.
Kwa kula sana parachichi husaidia mwili katika kazi yake ya kumeng"enya chakula vizuri na kuzuia urundikanaji mwingi wa vyakula visivyokua na kazi mwilini.kama tulivyoona hapo juu utumiaji wa mafuta yatkanayo na parachichi huchangia kwa kiasi kikubwa upungufu wa mafuta yaletayo lehamu na kuongeza mafuta yasiyo na lehamu.Hii hufanya mwili kujisikia mwepesi muda wote.Parachichi ina kiwango kikubwa cha kirutubisho cha fiba(nyuzinyuzi) ambacho huwa hakimeng"enywi tumboni lakini kikiwa na umuhimu mkubwa katika kusaidia kupata choo kizuri.

    AFYA YA NGOZI.
Tunafahamu kwamba ngozi ya binadamu huwa ina mafuta yake asili,bila kupaka mafuta ya kawaida hakumaanishi ngozi itakauka kabisa.ulaji wa parachichi huchangia ongezeko la mafuta asilia ndani ya mwili na kufanya ngozi kupata mafuta mengi ambayo hutumika kujilainisha kila itakapokauka.mafuta haya huipa ngozi muonekano mzuri na wenye afya.
Mbadala wa kula,mafuta yapatikanayo ndani ya parachichi huweza kupakwa katika ngozi kwa njia ya asili na mtu akajisikia murua.

    LISHE BORA KWA WALE WENYE KISUKARI.
Faida moja wapo ya chakula kutojirundika mwilini ni pamoja na kupunguza mrundikano wa sukari nyngi mwilini.Fiba ipatikanayo kwenye tunda hili husaidia mmeng"enyo wa chakula na kupunguza mrundikano wa sukari mwilini.Parachichi lina kiwango kidogo cha sukari na pia uwepo wa mafuta yake huchangia ufanyaji kazi mzuri wa homoni aina ya insulini katika urekebishaji wa sukari mwilini.

    MATATIZO YA UZAZI.
Ni dhahiri kwamba mtu mwenye matatizo ya moyo hukumbwa na matatizo ya uzazi pia,hii hutokana na kufanana kwa visababishi vya matatizo haya kwa namna moja ama nyngine.Hivyo unashauriwa kutumia tunda hili kwa kurekebisha na kuepuka sababu hizo.
Parachichi limeonyesha kuwa na faida kubwa katika kuboresha afya ya macho kwa uwepo wa vitamin A na vitamini nyingnezo kama vile E na C,pia husaidia kulainisha viungo vya mwili na kukufanya uwe mkakamavu muda wote kwani mafuta yapatikanayo kwenye tunda hili huongeza utepe kwenye jointi na kufanya mifupa kujongea vyema.Parachichi hutoa matokeo mazuri endapo litatumiwa kwa kufuata kanuni na taratibu husika za lishe.

   Usisite kuwasiliana nasi kwa ushauri,tiba na mapendekezo yoyote juu ya afya yako.
Wasiliana nasi kwa;

  Phone: 0673666791


Alhamisi, 5 Januari 2017

                Unaendeleaje ndugu msomaji wa AFYA KWANZA? Ni matumaini yangu nyote ni wazima wa afya.Tuchukue nafasi hii kumshukuru mungu kwa kutupa uhai na kutufanya kuendelea kuishi mpaka sasa.
Leo tuanze moja kwa moja na somo letu ambalo linahusiana na tunda mojawapo katika matunda ya hapo juu

NDIZI
Wengi tunalifahamu tunda hili na sio geni katika macho yetu,lakini linaweza likaw ni geni katika ufahamu wetu kutokana na kazi nyingi linazofanya tunda hili katika ujenzi na ulinzi wa afya yetu.Je tunafahamu kwamba ulaji wa ndizi mbivu mbili zitakuwezesha kufanya kazi kwa dakika 90 mfululizo?
      Kutokana na utafiti uliofanywa na taasisi ya afya nchini marekani,umebaini uwezo huo wa tunda la ndizi,(www.medical.news).
Ndizi ina aina fulani ya protini ijulikanayo kwa jina la TRYPTOPHAN ambayo hubadilishwa na kuwa SEROTON ambayo humfanya mtu ajisikie raha na amani ya akili hata kama ametoka kwenye msomgo wa mawazo.Tunashauri mtu kuacha kutumia vidonge vya kupunguza uchovu,pombe na hata sigara ili kujipa faraja na mapumziko ya akili lakini badala yake utumie tunda hili.

   MAUMIVU YA VIDONDA VYA TUMBO.

Ndizi huzuia maumivu yatokanayo na vidonda vya tumbo kwani hupunguza kasi ya uharibifu wa ukuta wa tumbo na tindikali inayozalishwa tumboni.

      SHINIKIZO LA DAMU.

 Ndizi pia husaidia kuweka sawa kiwango cha damu kwa kuongeza madini ya chuma pia husaidia kuweka sawa kiwango cha sukari kweny damu.hii hulifanya tunda hili kuwa na kazi ya kuratibu shinikizo la damu.Vilevile ndizi hutibu magonjwa ya figo na unashauriwa kutumia ndizi angalau moja kwenye milo yako kwa siku.Kwa uwezo huu wa ndizi,tunda hili linaweza kuwa moja ya dawa za kuzuia kama sio kuponya kabisa matatizo ya damu (anaemia).Wakina mama wengi wanashauriw kutumia ndizi kwani wanakutana na tatizo la upungufu wa damu mara nyingi.
    
   UWEZO WA KUFIKIRI.

Ndizi imekua ikiaminika sana katika kuongeza uwezo wa kufikiri baada ya jaribio kufanywa katika shule ya TWICKENHAM huko nchini uingereza,ambapo wanafunzi wapatao 200 walifanya tunda hili kuwa kama chakula cha mchana kwa muda upatao siku 40.Baada ya kufanya mitihani ikabainika kuwa wanafunzi hao ndio waliofaulu sana tofauti na wanafunzi wengine ambao hawakula ndizi.
Hii inatokana na ukweli kwamba,kuwepo na madini mengi ya aina ya potasium ndani ya tunda hili hufanya uwezo wa kufikiri kuamka na mwanafunzi kuchangamka.

   HANGOVER.

Ndizi huaminika sana kwa uwezo wake wa kuondoa uchovu utokanao na pombe ya jana,hii hutokana na uwezo wake wa kutuliza tumbo na mishipa ya fahamu.Juice ya mchanganyiko wa ndizi,asali pamoja na maziwa hufanya kazi hii.Tunashauri mtu kutumia glasi moja ya juisi hii ili kukata uchovu huo.
    Mbali na magonjwa hayo,ndizi pia imeaminika kutibu magonjwa mbalimbali kama vile mapigo ya moyo,kuondoa wasiwasi na magonjwa yatokanayo na upungufu wa protini.
Ndizi ikilinganishwa na matunda mengine huonekana kuwa na uwingi wa madini ya chuma na vitamini kwa wingi,pia inayo protini ya kutosha kuratibu mfumo mzuri ndani ya mwili.
  Fuata utaratibu mzuri wa ulaji wa ndizi ili uweze kupata matokeo bora ya afya yako.Tukutane muda na wakati mwingine Mungu akipenda.
Kwa ushauri na maoni wasiliana nasi kwa:
phone: 0673666791

Jumatano, 4 Januari 2017

Habari za muda huu ndugu msomaji,naamini u mzima wa afya na furaha hivyo huna budi kumshukuru Mungu.Kwa wale walio na matatizo ya kiafya na kiakili nao hawana budi kumshukuru mungu kwani pumzi waliyopewa kwa siku ya leo inatosha kabisa kusema asante kwa Mungu wako.
          Tuanze makala yetu kwa kuangalia virutubisho vinavyohitajika na mwili ili kuweza kukua na kustawi vizuri.Kama utakumbuka vizuri katika makala iliyopita nilishauri matumizi ya virutubisho asilia(natural) na siyo vya kutengenezwa(artificial).Virutubisho hivi ni muhimu kutumika kwani havina nyongeza ya kitu chochote ambacho kitatishia afya yako tofauti na virutubisho vya kutengenezwa ambavyo huwa na nyongeza ya vitu mbalimbali kama vle sukari,chumvi,rangi pamoja na dawa za kuhifadhia virutubisho hivyo.
Mwili wa binadamu yoyote unahitaji WANGA(carbohydrate) kwaajili ya kuupa nguvu zitakazo muwezesha kufanya jambo lolote,unahitaji PROTINI (protein) kwaajili ya kukua,unahitaji pia VITAMINI(vitamins) kama virutubisho vya kuchangia shughuli mbalimbali ndani ya mwili.Tusisahau pia mwili unahitaji FATI/MAFUTA(fatty/lipids) kwaajili ya kukinga viungo vya ndani(organs) na baridi pamoja na kuzalisha joto.
       Tutazungumzia umuhimu wa vitu vyote hapo juu kila tutakapokutana na kwaleo tuanze na virutubisho aina ya VITAMINI.
Tunaposema vitamini tunamaanisha ni aina mojawapo ya virutubisho ambavyo mwili huitaji kwaajili ya kufanya kazi mbalimbali,kwamfano ili mwili uweze kutengeneza seli hai mpya ni lazima ipate virutubisho vitakavyofanya kazi ya kuanzisha zoezi hilo.
Vitamini hupatikana katika vyakula tunavyokula kila siku,ndio maana tangu mwanzo tuliona kuna umuhimu wa kula CHAKULA BORA na sio BORA CHAKULA.Utakapokula chakula kilichokamilika chenye virutubisho vyote utajihakikishia afya iliyo imara na hautakua na hofu ya magonjwa nyemelezi.
        Vitamini hupatikana sana katika matunda na mbogamboga,hii inatuonyesha umuhimu wa ulaji wa matunda na mbogamboga za majani ili kuvipata virutubisho hivyo.Tumshukuru Mungu ndani ya nchi yetu Tanzania tumepata neema ya kuwa na matunda ya aina mbalimbali pamoja na mboga za majani.Pia tuipongeze serikali yetu kwa kuhamasisha kilimo sio cha mazao ya nafaka,pia hata kilimo cha matunda na mbogamboga.Hii inaonyesha uelewa wa viongozi wetu katika kuwajali watu wake pamoja na afya zao.
        Matunda yapo ya aina mbalimbali kama vile NDIZI,MAPAPAI,MACHUNGWA,MAEMBE nk....na kila aina ya matunda hutofautiana na aina ya vitamini zilizopo ndani yake.
Kutokana na kanuni za afya matunda ni kitu muhimu sana na inashauriwa kula matunda kwenye kila mlo kwa siku nzima.Ni vyema kula matunda kabla ya chakula na pia ni vyema kula matunda kama kifungua kinywa chako mara baada ya kuamka.KWANINI?
Kanuni hizo mbili za tulizoziona hapo juu zina umuhimu wake mkubwa katika afya yako,tutakuja kuziona kipindi kijacho kama Mungu akipenda iwe ivyo
Nikutakie siku njema katika kufuata kanuni za afya yako ili uepuke magonjwa nyemelezi.
Kwa ushauri,maonina mapendekezo usisite kuwasilina nasi kwa njia hapo chini,muda wowote na saa yoyote,tupo kwaajili ya kusaidia.

Wasiliana nasi kwa;
    Phone: 0673666791
    Email: goldamplat@gmail.com

Jumanne, 3 Januari 2017

   Habari za muda huu ndugu msomaji,ni matumaini yangu u mzima wa afya na furaha.Hatuna budi kumshukuru Mungu kwa hali kama hii,pia kama ni mgonjwa na una matatizo ya afya unapaswa kumshukuru Mungu pia.
Pole kwa wenye matatizo mbalimbali nawasihi msikate tamaa bali endelea kujituma ili ukabiliane nalo,kwani changamoto zinakuinua na kukukfikish sehemu fulani
     Lengo langu leo nataka kukupa jambo muhimu katika maisha yako ambapo ukilielewa na kulifuata vizuri utaishi kwa furaha,amani na pasipo kupatwa na maradhi kwa muda mrefu.
     TUNAKULA ILI TUISHI na sio TUNAISHI ILI TULE,hivyo basi unatakiwa kuangalia ni nini unakula kitakachokufanya uishi salama.Siku zote chakula unachokula ndicho kinachoamua uendelee kuishi kwa muda gani.Tazama kuna mifano mingi ya watu walioishi zamani ambao walifuata kanuni na taratibu za milo sahihi na wakaishi muda mrefu,hata uzee ulipowafikia uliwakuta wakiwa nguvu zao.Mtindo wa maisha wa sasa umebadilika sana ukilinganisha na wa zamani,kwani kuna utofauti mkubwa kati ya watu walioishi miaka ya zamani na tunaoishi miaka ya sasa.Kuanzia kwenye kufikiri,kutenda kazi na muda wa kuishi vyote vimebadilika sana,hii imetokana na mtindo wa maisha ambao tumechagua kuishi ambao ni tofauti sana na ule wa zamani.
Sababu kubwa ambayo tutajifunza ni CHAKULA kwani imechukua asilimia kubwa ya maisha yetu.
     Ili uweze kuwa na afya bora ni lazima upate chakula bora,namaanisha chakula safi,kilichokamilika kwa kila virutubishio.Ni vizuri zaidi kupata chakula asilia kwani kina uhakika mwingi wa virutubisho asilia,pia sio vibaya kutumia vyakula vilivyoongezewa virutubisho.Naomba nieleweke kitu kimoja hapa naongelea vyakula vilivyoongezewa virutubisho na siyo vilivyoongezewa rangi,ladha au sukari.Ninaposema virutubisho namaanisha ni vile vitu ambavyo mwili unahitaji kwaajili ya kujijenga vizuri kwa kupambana na magonjwa,kukua na kuimarika.Unapopata chakula bora unajihakikishia usalama wa maisha yako na kujiongezea muda mrefu wa kuishi bila tatizo la kiafya,hii itatokana na kufuata kanuni za afya ambazo utazipata kupitia ukurasa huu,hivyo nakusihi fuatana na mimi ili tujulishane na kuelekezana vitu mbalimbali vinavyohusu afya zetu kwa ujumla.
    Jiandae kujua mambo mbalimbali yanayokuhusu kwa namna moja au nyingine,au kama sio wewe hata ndugu na marafiki zako ili ukitoka hapa ukawaelekeze nn wanatakiwa kufanya ili wawe na afya bora na waishi miaka mingi kama wakifuata taratibu za afya.
Nitakaribisha maswali,maoni,ushauri na mtazamo wako,pia kwa ww ambaye utakua na tatizo la kiafya na unahitaji kusaidiwa kwa tiba usisite tuwasiliane kwa njia hapo chini.
Mungu awabariki,tukutane wakati ujao:
Phone: 0673666791
Email: goldamplat@gmail.com