Ijumaa, 3 Februari 2017

APPLE (TUFAA)

    Habari za muda huu ndugu mfuatiliaji wa makala haya,ni matumaini yangu u mzima wa afya na kama una matatizo ya kiafya,kiroho na hata mengine yatofautianayo na hayo ni wakati wako kumgeukia mungu na kumuomba akupe njia ya kuweza kukabiliana nayo.

Leo nimewiwa kukuletea matumizi sahii ya matunda katika afya zetu dhidi ya kujikinga na kupambana na magonjwa mbalimbali na tutaangalia umuhimu wa tunda aina ya apple (tufaa).Je unakumbuka ile kauli ya APPLE EATING KEEPS AWAY FROM DOCTOR? Basi kama hukumbuki basi ndivyo ilivyo na ni kweli kutokana na kazi nzuri zifanywazo nz tunda hili.

    Matufaa yana Vitamini K,nyuzinyuzi za chakula pamoja na dawa-lishe (phytochemicals) aina ya quercetin flavonoid hivyo kukuwezesha kupata virutubisho sahihi vinavyohitajika na mwili wako.matatizo mengi huondolewa na tunda hili na kukufanya uwe na mwili mwepesi pamoja ana afya njema kama utafuata taratibu za lishe katika matunda haya.Tuangalie faida zake kiafya;

HUREKEBISHA AFYA YA MAPAFU.
 Katika matunda ambayo yana mchango mkubwa juu ya magonjwa na matatizo ya mapafu ni pamoja na tunda hili,umaarufu wake umetokana na kazi kubwa ya kurekebisha maswala ya mapafu.Majimaji yaliyopo kwenye apple yana mchango mkubwa sana juu ya kuondoa bakteria ambao wanavamia mapafu na kuleta magonjwa kama kifua kikavu.
Kuna asilimia kubwa kwa apple kutibu kansa ya mapafu kutokana na kazi za kuzuia maambukizi ndani ya mapafu,wataalamu wengi wameshauri kula tunda hili kwa lengo la kurekebisha afya yako ya mwili mzima kiujumla.

HUZUIA MAWE KWENYE FIGO.
 Kwa kurekebisha mzungoko mzuri wa damu mwilini,apple linauwezo mkubwa wa kusafisha damu yako na kufanya ini pampja na figo kupunguziwa kazi ya kuchuja taka mwili ndani ya mwili.Magonjwa ya ini na figo huzuiliwa kwa tunda hili la apple.

SOLIDI YA TUMBO (COLITIS).
 Kama unasumbuliwa na tumbo la kuhara na hujisikii vizurim kila baada ya kula unashauriwa kuanza mara moja kutumia tunda hili kama kinga kwani linasaidia katika kurekebisha udhaifu wowote wa tumbo.
Ulaji wa apple unatia nguvu mwili na kukufanya kukaa muda mrefu bila kusika njaa au uchovu.Ma apple matatu yanakufanya kukaa masaa nane pasipo kuhisi uchovu mwilini mwako na kukuweka active kwa muda wote huo.

MAGONJWA YA KUHARISHA.
 Hii huonekana katika mambo yote mawili kwenye kuharisha au kupata choo kigumu nyuzi nyuzi zilizopo ndani ya tunda hili kama kwenye matunda mengine tuliyoyaona hapo awali,zitakufanya uondokane na tatizo kama hili.
Tumia kwa lengo la afya na sio kwa mazoea kama kusitisha matumizi au kula ukijisikia kufanya hivyo kwani hutaona manufaa yoyote na utaishia kulalamika kwamba hujapata matokeo mazuri.

MATATIZO YA DAMU.
 Matatizo kama blood pressure na anaemia hurekebishwa kwa ulaji wa matunda haya kwani lina kiwangi kikubwa cha calcium 10mg ambacho huweka sawa uwiano wa minerals zipatikanazo ndani ya damu.hupunguza kiasi cha Nacl ambacho hutofautisha na kufanya pressure ipande kwa kiasi kikubwa katika damu na kurudisha uwiano sawa 
 Kwa uwingi wa iron na arsenic pamoja na phosphorus husaidia kuongeza madini muhimu katika kurekebisha damu yako mwilini.

NB: Ulaji wa apple moja kwa siku ni zaidi ya mtu aliyekula mikate mitano isiyotiwa amira.

  Ulaji wa matunda haya kila siku utakufanya umsahau daktari na kukuweka mbali na hospitali,pia utamsababishia daktari kukosa ajira yake.
Nakushauri kuanza leo kutmia tiba hizi ili iwepo tofauti kati yako wewe na mtu ambaye alipuuzia ili apate mfano kwako jinsi ya afya yako itakavyokua bora.
Usisite kuwasiliana nasi muda na saa yoyote kama uan swali au maoni yoyote kuhusiana na afya yako...Ahsante

PHONE:  0673666791

Email: goldamplat@gmail.com

Jumatano, 1 Februari 2017

ZAITUNI.


   U hali gani ndugu msomaji wa makala haya ya AFYA KWANZA,ni matumaini yangu uko poa na mwenye afya njema tunapaswa kwa pamoja kumshukuru mungu kwa kutufanikishia jambo hilo.

     Leo tena ni siku nyingine ambayo tutaeleweshana kuhusu mambo fulani yahusuyo afya zetu kutokana na ulaji wa tunda aina ya zaituni.Tunda hili linaweza lisijulikane na wengi miongoni mwetu kwani linaoatikana kwa asilimia ndogo nchini ketu lakini limeonekana kuwa na kazi nyingi muhimu katika miili yetu.Tuangalie baadhi ya kazi zake hizo ni kama ifuatavyo:

HUPUNGUZA UZITO
 Tunda la zaituni limekua likiorodheshwa sana kwenye lishe za kupunguza uzito/unene,hii ni kutokana na ukweli kwamba tunda hili lina mafuta (olive oil) mepesi ambayo hayawezi kuganda ndani ya mwili na matumizi yake hutumika haraka baada ya kuonekana ndani ya mwili.Kwa watu wenye uzito uliopitiliza niwashauri kuanza kutumia tunda hili.

KUONGEZA NGUVU ZA KIUME.
 Kutokana na kurekebisha afya ya damu mwilini na kukupa nguvu ya mzunguko mpya mwilini,hamu na uwezo wa kimapenzi huongezeka ndani ya mwili wa mtumiaji wa tunda hili.Kutokana na uwezo huo watu wamekua wakilisifia tunda hilo kwa kazi yake hiyo kubwa bila kujua linafanya nini kukamilisha kazi hiyo.

TATIZO LA MAFUA.
 Wengine hutumia mafuta ya mizeituni (olive oil) kupaka kwenye upeo wa eneo la mbele ya pua kama dawa ya kutibu ugonjwa wa mafua,lakini mpaka sasa bado haijafahamika wazi ni kwanini mafuta haya hutibu mafua kwa dizaini kama hiyo ya VIKS-KINGO.

MAGONJWA YA NGOZI.
Hii ni kweli na inasaidia kwa kiasi kikubwa sana kwa mtumiaji kwani tunda la zaituni lina kiwango kikubwa sana cha vitamin D ambayo ndiyo hasa hutumika katika kurekebisha matatizo ya ngozi.Paka mafuta ya mizeituni na utaona tofauti ndani ya muda mchache

HUREKEBISHA TATIZO LA NYWELE.
 Kwa wale wenye nywele za kukatika na zilizojikunja,unaweza kutumia mafuta haya kwa kuzirefusha na kuzuia zisijikunje tena,vitamini D iliyopo ndani ya tunda hili husaidia kwa kiasi kikubwa kurekebisha afya ya ngozi kwenye kichwa ambayo huruhusu ukuaji mzuri wa mizizi ya nywele.Unaweza kuona wazi kwamba mafuta mazuri ya nywele ni OLIVE OIL.
            NB: Isionekane kama nafanya promotion ya baadhi ya mafuta ya nywele na vipodozi,Hapana.

HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KANSA
Mafuta ya zeituni (olive oil) yana olecanthal na of mimics inayozalisha ibuprofen inayosaidia  kupunguza hatari ya kupata cancer.Ni mafuta mazuri kwa yule atakaye jali afya ya mwili wake na kuitetea na ifahamike wazi kwamba wapo wagonjwa wa kansa ambao wanatumia mafuta ya mizeituni katika mlo wao wa kila siku kama kupunguza /kufisha sumu ya kansa mwilini.

NI DAWA SAHIHI YA UBONGO.
 Hii ni kwa watoto wadogo ambao wanakua,virutubisho vipatikanavyo kwenye mafuta ya tunda hili likiwa bado halijapikwa ni muhimu sana ukilinganisha na vile ambavyo hupatikana baada ya kuyapika mafuta hayo.Muanzishie mwanao utaratibu wa kumnywesha mafuta mabichi ya mzeituni ili kulinda afya yake na kumfanya awe mchangamfu na mwenye akili timamu.

DAWA YA MASIKIO KWA WATOTO WADOGO.
 Watoto wenye matatizo ya masikio kama kuwashwa mara kwa mara na kutokwa na uchafu mwingi mwilini wnaweza wakaondokana na tatizo hilo kwa kumuanzishia dozi ya mafuta hayo.Matone mawili mpaka matatu mara mbili kwa siku kutafanya tatizo hili kupotea kabisa.
Ifahamike wazi kwamba mafuta ya mzeituni (olive-oil) baada ya kupikwa hupoteza ubora wake na kutengeneza sumu lishe ambazo zitatolewa nje ya mwili bila kufanya kazi yoyote.Hivyo basi ni muhimu kuanzisha utaratibu wa kutumia mafuta mabichi ya mizeituni kuliko kuya[pika kwanza.

Kwa ushauri na maswali kuhusiana na tatizo lolote linanalo kusibu,usisite kuwasiliana nasi kwa namba hizo apo chini,,,,,Ahsante.

         Pia kuna matumizi ya kiimani kuhusiana na mafuta yatokanayo na matunda haya.
    NB: Ikumbukwe kwamba hatutolei mafunzo ya afya kwanza kutokana na imani ya mtu fulani,bali hata wasioamini nao wana haki katika jamii inayowazunguka.

                       PHONE:  0624259822

Jumatatu, 30 Januari 2017

  UKWAJU.


    Habari ndugu mpenzi msomaji wa makala haya,nakukaribisha tena ili kufahamu umuhimu wa tunda lingine aina ya Ukwaju.Ni tunda la tofauti kidogo kati ya matunda mengine ambayo tumekwisha yaona hapo awali lakini leo ngoja tuangalie umuhimu wa utofauti wake na matunda mengine.

    Kidogo ni tunda la kushangaza kwani lina ladha tamu na chachu,tunda hili unapoanza kula kwanza lazima likusisimue ndipo uendano nalo na imekua ni vigumu kwa watoto wadogo kulila tunda hili wenyewe kama wenyewe kutokana na ladha yake.Ulaji wake haujatofautiana na matunda mengine kwani unaweza kulila kama tunda,ukatengeneza juisi na ukanywa na hata ukatumia kama siagi.Kusema kweli ni tunda lenye maana kubwa kutokana na kazi lilizokua nalo,tuangalie baadhi ya kazi hizo ni kama ifuatavyo.

HUTIBU HOMA.
 Kuanzia homa ya tumbo mpaka homa ya manjano tunda hili hutibu pasipo kuangalia.Hii ni kutokana na asidi liyopo ndani ya tunda hili inayozuia kabisa uzalianaji wa bacteria hatari ndani ya tumbo na kuwaacha wale wanaohitajika kubaki tuu.Imetumika kama dawa yenye manufaa zaidi kwani mtu akiumwa tumbo na kutumia ukwaju basi amejihakikishia pona yake.

HUSAIDIA USAGAJI WA CHAKULA.
 Kama yalivyo matunda mengine,ukwaju una nyuzi nyuzi ambazo husaidia katika usagaji wa chakula na kukupa choo kizuri kama tulivyoona katika matoleo ya nyuma.Kwa mwenye tatizo kama hili hatakiwi kuuliza afanye nini ili aweze kujiponya wakati dawa ya ukwaju tayari ipo na inapatikana sokoni.

HUTIBU VIDONDA.
 Vidonda vya kuungua hupona kwa kutumia ukwaju,lakini mara nyingi hutokana baada ya mchanganyiko wa tunda hili na asali.Mchanganyo utakaotumika kama dawa unatofautiana kulingana na sehemu ya jeraha au ukubwa wa jeraha pia.

HUTIBU MAAMBUKIZI YA KOO.
 Bakteria pamoja na protozoa wengine wanaoshambulia mfumo wa upumuaji huzuiwa kufanya hivyo mara tuu wanapotaka kuingia kwenye sehemu za ndani kabisa za mfumo huo kutokana na asidi inaypatikana ndani ya tunda hili,hii itakuweka huru na magonjwa yote ya koo na hata ya mfumo wa chakula kwani ni koo hilohilo ndilo linalounganisha mifumo hiyo miwili.

HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KANSA.
 Tunda la ukwaju limewasaidia wengi katika kurekebisha afya zao na kupunguza uwezekano mkubwa wa kupata kansa kwani ladha yake ya uchachu hairuhusu ukuaji wa kansa mwilini.Unashauriwa kutumia mara kwa mara ili kupunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kupata kansa mwilini mwako.Kinga za ukwaju zitazuia ukuaji wa kansa kama zitapatikana kwa wingi mwilini mwako na si vinginevyo.

UKOSEFU WA HAMU YA KULA.
 Kwa wale wanaokosa hamu ya kula chakula,tunda la ukwaju ni msaada mzuri kukurejesha katika hali yako madhubuti.Ingawa watoto wengi hukumbwa na tatizo hili pale ambapo wanakua au wamepatwa na homa,andaa juisi yako ya ukwaju na kisha tumia kikombe kimoja nusu saa kabla ya kula utaona mafanikio.

    kutokana na kazi hizo,tunashauri tunda la ukwaju lisikose katika mlo wako wa kila siku kwani lin kazi kubwa sana ukilinganisha na matunda mengine ingawa baadhi zinafanana.Tumia ukwaju kama dawa kama ninavyokwambia kwenye matunda mengine na sio utumie pale ambapo unaona tatizo limekufika kwani hata kama utapata mafanikio hayatakua makubwa kwani matunda mengi ni kinga dhidi ya magonjwa na machache ni dawa hivyo unapaswa kutumia kwa kujitaadharisha na magonjwa yajayo.

  Kama utakua unafanya hivyo kwa utaratibu wa kujiwekea ulinzi na akiba ya kinga mwilini utakua mbali kiafya na hautasumbuliwa na magonjwa nyemelezi kirahisi,lakini hakikisha unamshauri na ndugu au rafiki na hata mwenzako uliye nae jirani kufuata kanuni na taratibu za afya ili aepukane na magonjwa.
  Sina la ziada kwa siku ya leo,kwa maswali juu ya afya yako na ushauri wowote usisite kuwasiliana nasi tutakusaidia vyema kwa wakati wowote na muda wowote.Ahsante

Kwa mawasiliano usisite kututafuta;

  PHONE : 0673666791

  Email:  goldamplat@gmail.com