Ijumaa, 3 Februari 2017

APPLE (TUFAA)

    Habari za muda huu ndugu mfuatiliaji wa makala haya,ni matumaini yangu u mzima wa afya na kama una matatizo ya kiafya,kiroho na hata mengine yatofautianayo na hayo ni wakati wako kumgeukia mungu na kumuomba akupe njia ya kuweza kukabiliana nayo.

Leo nimewiwa kukuletea matumizi sahii ya matunda katika afya zetu dhidi ya kujikinga na kupambana na magonjwa mbalimbali na tutaangalia umuhimu wa tunda aina ya apple (tufaa).Je unakumbuka ile kauli ya APPLE EATING KEEPS AWAY FROM DOCTOR? Basi kama hukumbuki basi ndivyo ilivyo na ni kweli kutokana na kazi nzuri zifanywazo nz tunda hili.

    Matufaa yana Vitamini K,nyuzinyuzi za chakula pamoja na dawa-lishe (phytochemicals) aina ya quercetin flavonoid hivyo kukuwezesha kupata virutubisho sahihi vinavyohitajika na mwili wako.matatizo mengi huondolewa na tunda hili na kukufanya uwe na mwili mwepesi pamoja ana afya njema kama utafuata taratibu za lishe katika matunda haya.Tuangalie faida zake kiafya;

HUREKEBISHA AFYA YA MAPAFU.
 Katika matunda ambayo yana mchango mkubwa juu ya magonjwa na matatizo ya mapafu ni pamoja na tunda hili,umaarufu wake umetokana na kazi kubwa ya kurekebisha maswala ya mapafu.Majimaji yaliyopo kwenye apple yana mchango mkubwa sana juu ya kuondoa bakteria ambao wanavamia mapafu na kuleta magonjwa kama kifua kikavu.
Kuna asilimia kubwa kwa apple kutibu kansa ya mapafu kutokana na kazi za kuzuia maambukizi ndani ya mapafu,wataalamu wengi wameshauri kula tunda hili kwa lengo la kurekebisha afya yako ya mwili mzima kiujumla.

HUZUIA MAWE KWENYE FIGO.
 Kwa kurekebisha mzungoko mzuri wa damu mwilini,apple linauwezo mkubwa wa kusafisha damu yako na kufanya ini pampja na figo kupunguziwa kazi ya kuchuja taka mwili ndani ya mwili.Magonjwa ya ini na figo huzuiliwa kwa tunda hili la apple.

SOLIDI YA TUMBO (COLITIS).
 Kama unasumbuliwa na tumbo la kuhara na hujisikii vizurim kila baada ya kula unashauriwa kuanza mara moja kutumia tunda hili kama kinga kwani linasaidia katika kurekebisha udhaifu wowote wa tumbo.
Ulaji wa apple unatia nguvu mwili na kukufanya kukaa muda mrefu bila kusika njaa au uchovu.Ma apple matatu yanakufanya kukaa masaa nane pasipo kuhisi uchovu mwilini mwako na kukuweka active kwa muda wote huo.

MAGONJWA YA KUHARISHA.
 Hii huonekana katika mambo yote mawili kwenye kuharisha au kupata choo kigumu nyuzi nyuzi zilizopo ndani ya tunda hili kama kwenye matunda mengine tuliyoyaona hapo awali,zitakufanya uondokane na tatizo kama hili.
Tumia kwa lengo la afya na sio kwa mazoea kama kusitisha matumizi au kula ukijisikia kufanya hivyo kwani hutaona manufaa yoyote na utaishia kulalamika kwamba hujapata matokeo mazuri.

MATATIZO YA DAMU.
 Matatizo kama blood pressure na anaemia hurekebishwa kwa ulaji wa matunda haya kwani lina kiwangi kikubwa cha calcium 10mg ambacho huweka sawa uwiano wa minerals zipatikanazo ndani ya damu.hupunguza kiasi cha Nacl ambacho hutofautisha na kufanya pressure ipande kwa kiasi kikubwa katika damu na kurudisha uwiano sawa 
 Kwa uwingi wa iron na arsenic pamoja na phosphorus husaidia kuongeza madini muhimu katika kurekebisha damu yako mwilini.

NB: Ulaji wa apple moja kwa siku ni zaidi ya mtu aliyekula mikate mitano isiyotiwa amira.

  Ulaji wa matunda haya kila siku utakufanya umsahau daktari na kukuweka mbali na hospitali,pia utamsababishia daktari kukosa ajira yake.
Nakushauri kuanza leo kutmia tiba hizi ili iwepo tofauti kati yako wewe na mtu ambaye alipuuzia ili apate mfano kwako jinsi ya afya yako itakavyokua bora.
Usisite kuwasiliana nasi muda na saa yoyote kama uan swali au maoni yoyote kuhusiana na afya yako...Ahsante

PHONE:  0673666791

Email: goldamplat@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni