Jumatano, 1 Februari 2017

ZAITUNI.


   U hali gani ndugu msomaji wa makala haya ya AFYA KWANZA,ni matumaini yangu uko poa na mwenye afya njema tunapaswa kwa pamoja kumshukuru mungu kwa kutufanikishia jambo hilo.

     Leo tena ni siku nyingine ambayo tutaeleweshana kuhusu mambo fulani yahusuyo afya zetu kutokana na ulaji wa tunda aina ya zaituni.Tunda hili linaweza lisijulikane na wengi miongoni mwetu kwani linaoatikana kwa asilimia ndogo nchini ketu lakini limeonekana kuwa na kazi nyingi muhimu katika miili yetu.Tuangalie baadhi ya kazi zake hizo ni kama ifuatavyo:

HUPUNGUZA UZITO
 Tunda la zaituni limekua likiorodheshwa sana kwenye lishe za kupunguza uzito/unene,hii ni kutokana na ukweli kwamba tunda hili lina mafuta (olive oil) mepesi ambayo hayawezi kuganda ndani ya mwili na matumizi yake hutumika haraka baada ya kuonekana ndani ya mwili.Kwa watu wenye uzito uliopitiliza niwashauri kuanza kutumia tunda hili.

KUONGEZA NGUVU ZA KIUME.
 Kutokana na kurekebisha afya ya damu mwilini na kukupa nguvu ya mzunguko mpya mwilini,hamu na uwezo wa kimapenzi huongezeka ndani ya mwili wa mtumiaji wa tunda hili.Kutokana na uwezo huo watu wamekua wakilisifia tunda hilo kwa kazi yake hiyo kubwa bila kujua linafanya nini kukamilisha kazi hiyo.

TATIZO LA MAFUA.
 Wengine hutumia mafuta ya mizeituni (olive oil) kupaka kwenye upeo wa eneo la mbele ya pua kama dawa ya kutibu ugonjwa wa mafua,lakini mpaka sasa bado haijafahamika wazi ni kwanini mafuta haya hutibu mafua kwa dizaini kama hiyo ya VIKS-KINGO.

MAGONJWA YA NGOZI.
Hii ni kweli na inasaidia kwa kiasi kikubwa sana kwa mtumiaji kwani tunda la zaituni lina kiwango kikubwa sana cha vitamin D ambayo ndiyo hasa hutumika katika kurekebisha matatizo ya ngozi.Paka mafuta ya mizeituni na utaona tofauti ndani ya muda mchache

HUREKEBISHA TATIZO LA NYWELE.
 Kwa wale wenye nywele za kukatika na zilizojikunja,unaweza kutumia mafuta haya kwa kuzirefusha na kuzuia zisijikunje tena,vitamini D iliyopo ndani ya tunda hili husaidia kwa kiasi kikubwa kurekebisha afya ya ngozi kwenye kichwa ambayo huruhusu ukuaji mzuri wa mizizi ya nywele.Unaweza kuona wazi kwamba mafuta mazuri ya nywele ni OLIVE OIL.
            NB: Isionekane kama nafanya promotion ya baadhi ya mafuta ya nywele na vipodozi,Hapana.

HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KANSA
Mafuta ya zeituni (olive oil) yana olecanthal na of mimics inayozalisha ibuprofen inayosaidia  kupunguza hatari ya kupata cancer.Ni mafuta mazuri kwa yule atakaye jali afya ya mwili wake na kuitetea na ifahamike wazi kwamba wapo wagonjwa wa kansa ambao wanatumia mafuta ya mizeituni katika mlo wao wa kila siku kama kupunguza /kufisha sumu ya kansa mwilini.

NI DAWA SAHIHI YA UBONGO.
 Hii ni kwa watoto wadogo ambao wanakua,virutubisho vipatikanavyo kwenye mafuta ya tunda hili likiwa bado halijapikwa ni muhimu sana ukilinganisha na vile ambavyo hupatikana baada ya kuyapika mafuta hayo.Muanzishie mwanao utaratibu wa kumnywesha mafuta mabichi ya mzeituni ili kulinda afya yake na kumfanya awe mchangamfu na mwenye akili timamu.

DAWA YA MASIKIO KWA WATOTO WADOGO.
 Watoto wenye matatizo ya masikio kama kuwashwa mara kwa mara na kutokwa na uchafu mwingi mwilini wnaweza wakaondokana na tatizo hilo kwa kumuanzishia dozi ya mafuta hayo.Matone mawili mpaka matatu mara mbili kwa siku kutafanya tatizo hili kupotea kabisa.
Ifahamike wazi kwamba mafuta ya mzeituni (olive-oil) baada ya kupikwa hupoteza ubora wake na kutengeneza sumu lishe ambazo zitatolewa nje ya mwili bila kufanya kazi yoyote.Hivyo basi ni muhimu kuanzisha utaratibu wa kutumia mafuta mabichi ya mizeituni kuliko kuya[pika kwanza.

Kwa ushauri na maswali kuhusiana na tatizo lolote linanalo kusibu,usisite kuwasiliana nasi kwa namba hizo apo chini,,,,,Ahsante.

         Pia kuna matumizi ya kiimani kuhusiana na mafuta yatokanayo na matunda haya.
    NB: Ikumbukwe kwamba hatutolei mafunzo ya afya kwanza kutokana na imani ya mtu fulani,bali hata wasioamini nao wana haki katika jamii inayowazunguka.

                       PHONE:  0624259822

Maoni 1 :