Alhamisi, 26 Januari 2017

ZABIBU.




     Ni matumaini yangu u mzima wa afya na unaendelea na majukumu yako ya kila siku katika kujenga nchi yenye nguvu.Nchi imara haiwezi kuja kama wajenzi wake wana afya dhaifu itakua ni dhahania hivyo hakikisha unafuata kanuni za mlo wa afya na kinga mwilini mwako ili kupata afya iliyo thabiti.
  Leo mezani kwangu nimekuandalia tunda lingine ambalo ni moja kati ya tunda la karne na karne lenye sifa na uwezo mkubwa,nalo si lingine bali ni Zabibu.

  Katika matunda yaliyojizolea umaarufu mkubwa kuanzia karne ya sita ni tunda hili.ni la zamani sana na lilitumika kutengenezea pombe (mvinyo) tangu enzi za watu wa kale.Kusema ukweli tunda hili ni tamu na linapendwa na kila mtu hasa hasa na watoto.
  Kuna aina tatu ya zabibu nayo ni zabibu za kijani,nyekundu na kama nyeusi (dark-red),aina zote hizi huliwa kwa njia mbalimbali kama vile kwa kutengenezewa juisi,zabibu zilizo kaushwa kama raisin na kama tunda la kawaida  kama matunda mengine.Tuangalie faida kuu za tunda hili;

 VITAMINI B COMPLEX.
  Karibu aina zote za vitamini B unazozifahamu zipo humu kwenye zabibu,hii inalipa sifa tunda hili kurekebisha matatizo yote yarekebishwayo na vitamini hizi.Kuna kama vile magonjwa ya damu na mengineyo.

HUTIBU PUMU.
Tunda hili lina maji kiasi chacke ambayo kazi kubwa ni kuongeza unyevunyevu ndani ya mapafu na kupunguza uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa unaohusiana na njia hiyo ya hewa.Dawa nyingi za mitishamba ambazo hutumika kutibu pumu huchanganywa na unga wa zabibu zilizo sagwa na kukaushwa vizuri.

HUONDOA SUMU.
Viondoa sumu (anti-oxidants) ambavyo hupatikana kwenye tunda hili vina kazi kubwa sana kuachilia mbali nguvu inayotolewa kwenye maziwa.Mgonjwa ambaye amekunywa sumu mara tu na hakuna uwezekano wa maziwa jirani,unaweza kumpa juisi ya zabibu kama ipo jirani na hii itamsaidia.

HEREKEBISHA TATIZO LA DAMU.
Zabibu huongeza kiwango cha nitric acid mwilini ambacho huzuia damu kuganda.pia inaaminika kwamba juisi ya tunda hili inaongeza damu kwa mtumiaji anayeitumia mara kwa mara na husaidia kupunguza tatizo la moyo linalosababishwa na damu kuwa chache mwilini

HULAINISHA CHOO.
ukweli ni kwamba zabibu lina kiasi cha kawaida cha kamba lishe ambacho hufanya kazi ya kurekebisha choo kikubwa.Watoto wengi wanaokosa maji mwilini kutokana na wazazi kushindwa kuwapa maji ya kutosha,wanaweza kuanzishiwa utumiaji wa juisi ya tunda hili.

HUPUNGUZA MAFUTA MWILINI.
 Zabibu halina mafuta,hii husaidia kurekebisha uwingi wa mafuta yaliyomo ndani ya mwili kwani yana kiwango kikubwa cha carlories ambazo hushawishi matumizi ya mafuta kwa kuzalisha nguvu mwilini pindi ambapo zimekwisha carlories hizo.
  Tunda hili ni tamu na huweza kuliwa kwa kupitiliza kutokana na ladha yake,kumbuka kwa kufanya hivyo huendani na kanuni za afya bali unajiongezea uchafu mwilini kwani kiasi kidogo kinachohitajika kitachukuliwa na kilichobakia kitatolewa nje kama makapi ."Kula kwa afya na sio ule kwa kuwa kipo" nakumbuka zamani mama alikua anapenda sana kutumia maneno hayo akimaanisha nile kwa kiasi.

  Hata mimi leo sina budi kukushauri kwa matokeo thabiti ya afya yako tumia kiasi kidogo mara kwa mara kama ulivyoelekezwa hapo juu na hakika matokeo yake utayapata ndani ya muda mfupi.
Kwa ushauri,maoni au maswali kuhusiana na matatizo ya kiafya usisite kuwasiliana nasi kwa mawasiliano hapo chini....Ahsante.

PHONE;  0673666791

Email; goldamplat@gmail.com 

Jumatano, 25 Januari 2017

KAROTI.


          Habari ndugu mpenzi msomaji wa makala haya,nakukaribisha tena ili kufahamu umuhimu wa tunda lingine aina ya Karoti.Ni tunda la tofauti kidogo kati ya matunda mengine ambayo tumekwisha yaona hapo awali lakini leo ngoja tuangalie umuhimu wa utofauti wake na matunda mengine.
   Kwanza hili ni tunda pekee ambalo linaweza kupikwa na lisiharibu ladha yake,pia linaweza kuliwa likiwa kama matunda mengine yanavyoliwa bila kupikwa.Pia tunda hili ni moja wapo kati ya matunda machache ambayo yanaoatikana chini ya ardhi,tumezoea matunda mengi hupatikana juu ya miti au hata yakiwa yamelala ardhini lakini sio chini ya ardhi kwa kufanya kuyafukua/kuchimba.

  Kuna aina tatu za karoti ambazo hutofautiana kwa rangi zake,kuna karoti nyekundu,ya njano na ya pinki lakini zote ni karoti.Karoti za njano na nyekundu ndizo zenye virutubisho vingi ukilinganisha na hiyo ya pink na mara nyingi ndizo aina za karoti ambazo hulimwa sana nchini kwetu Tz.
    Karoti kama yalivyo matunda mengine lina faida kubwa sana nyingi,watu wengi tumekua tukisikia faida moja tuu ya kutibu macho na kuyafanya yawe maangavu.Ni kweli lakini siyo kazi hiyo tuu bali kuna kazi nyingi za aina mbalimbali,ungana nami tuzione hapo chini;

 HUTIBU MATATIZO YA CHOO.
  Karoti lina kiasi kikubwa cha kamba lishe ambazo ndizo muhimu katika kurekebisha tumbo na kukupatia choo kizuri.Kambalishe hizi husaidia katika ufyonzaji wa maji katika njia ya mwisho ya usagaji wa chakula hivyo kukuweka katika hali nzuri kama zitapatikana kwa kiasi kikubwa mwilini.

 HULAINISHA NGOZI.
  Kwa mtumiaji wa karoti mara kwa mara atakubaliana na mimi kwa kazi hii ambayo karoti inafanya,warembo wengi wanatumia mafuta na losheni za ngozi zilizotengenezwa na tunda hili kwaajili ya umakini wa ngozi zao.Hii inatokana na uwepo wa vitamini E iliyopo ndani ya karoti inayofanya kazi ya kurudisha na kutengeneza seli mpya za ngozi zilizo haribika/kufa.

 HUFANYA MACHO KUWA MAANGAVU.
  Karoti ina kirutubisho kiitwacho Beta-carotenene ambacho ndio chanzo muhimu cha vitamini A mwilini.Baada ya kubadilishwa na kuwa vitamini A mwilini,carotenene hupelekwa moja kwa moja katika utengenezaji wa seli ndani ya pupil na retina kwenye macho.Hii hufanya uwingi wa seli hizi na kusababisha kuondoa tatizo la kutokuona kwenye mwanga hafifu au mdogo.

 HUONDOA TATIZO LA CHUNUSI.
  Kama tulivyoona hapo juu vitamin E ndiyo hasa itumikayo kupambana na magonjwa ya ngozi,hivyo kwa uwepo wa vitamini hii hutatua tatizo la chunusi na vipele vitokanavyo na mafuta mengi usoni.

CHANZO CHA NISHATI MWILINI.
 Karoti haina mafuta bali ina karolies nyingi,hivyo kwa mtumiaji wa karati hupata virutubisho hivi kwa wingi na kumfanya awe na nguvu za kumwezesha kuhimili kazi mbalimbali.

 HUREKEBISHA TATIZO LA DAMU.
  Juisi ya karoti inasifika kurekebisha tatizo la upungufu wa damu mwilini,kwa matumizi ya kama dawa unashauriwa kutumia ndani ya muda wa si chini ya miezi mitatu.Kunywa glasi moja ya juisi kila siku kwa matatizo ya damu.

  Karoti ni muhimu sana kwa watoto wadogo kwani ina vitamini A nyingi ambazo zitamjengea mtoto kinga nzuri juu ya magonjwa mengine mengi tofauti na ya macho.Unashauriwa kumwanzishia mtoto wako mdogo utaratibu wa kunywa juisi ya karoti kama dawa kwa kumkinga na monjwa mengine mengi.
Tunda hili limekuwa na sifa nyingi kutokana na kazi yake kubwa moja ya kutibu macho.
   Kwa kuwa na viondoa sumu vingi ndani ya karoti,imekuwa na mchango mkubwa wa kutibu magonjwa ya kansa kama vile kansa ya mapafu,tumbo na tezi za uzazi za kiume.
Kwa faida nyingine nyingi tazama; http://www.a2ztube.co.
  Kwa lolote linakusumbua kuhusu afya yako usisite kuwasiliana nasi kwa ushauri na kukujibu maswali yako.Pia tunatoa huduma za kufundisha taratibu za milo mingine kwa ajili ya matatizo ya afya yatokanayo na mfumo wa maisha...Ahsante.

PHONE;  0673666791

Email: goldamplat@gmail.com

Jumapili, 22 Januari 2017

 TIKITI-MAJI.



     Leo tena katika makala nyingine tunakutana kuzungumzia tunda aina ya Tikiti-maji,kabla ya kuanza mada yetu hatuna budi kumshukuru Mungu kwa yote aliyotutendea na kutuweka salama mpaka muda huu.Ni matumaini yangu ni wazima wa afya na mmejaaliwa kuiona siku nyingine hivyo sifa na utukufu arudishiwe Mungu muweza yote.

  Kama wengi jinsi tunavyolifahamu tunda hili kuwa na uwingi wa 92% ya maji pekee ndivyo kazi yake kubwa yakuhakikisha maji mwilini mwa mtumiaji hayapungui.Tikiti-maji lina aina mbalimbalio za madini ambayo hufanya kazi nyingi mwilini mwetu na kusaidia kuboresha afya ya mlaji.
Tuangalie baadhi ya kazi muhimu za tunda hili;

HUONGEZA NGUVU ZA KIUME.
 Kila kipatikanacho ndani ya tunda hili kina kazi kubwa ukianzia majani,maganda pamoja na mbegu.Wanaume wengi wamekua wakikumbwa na tatizo la hili na kumekuwa na matangazo mbalimbali kuhusiana na dawa za kusaidia tatizo hili.Ndugu msomaji ni bora kutumia dawa za matunda/lishe ili kutibu au kupunguza au kuzuia tatizo lako na sio kila dawa kuiona inafaa.Mbegu za tunda hili zikiliwa pamoja na nyama ya tunda hili husaidia katika kurekebisha upungufu wa nguvu za kiume kwa asilimia kubwa kuliko inavyotegemewa.Watu wengi wamejaribu kufanya hivyo na matokeo wamerudisha sifa na shukrani kwa somo hilo,tuwasiliane kwa maelezo zaidi.

HUONDOA SUMU MWILINI.
  Lycopene ipatikanayo ndani ya tunda hili husaidia kuzuia sumu mbalimbali mwilini zisiudhuru.Pia sumu zipatikanazo kwenye baadhi ya nyama (protini) hurekebishwa kwa kirutubisho hiki.Pia baadhi ya protini ngumu tunazokula kila siku husagwa nakufanywa nyepesi kuchukuliwa ndani ya mwili na kufanya kazi husika kuliko kutolewa nje kama uchafu/kinyesi.

HUSAIDIA MATATIZO YA CHOO NA UPUNGUFU WA MAJI.
 Kuwepo kwa maji kwa asilimia nyingi pamoja na kamba lishe,kunasaidia kurekebisha matatizo ya choo na kibofu cha mkojo.Kwa wenye magonjwa haya,kwa kutumia tunda la Tikiti-maji wataweza kuyatibu na kuyazuia na kwa wale ambao hawana wanashauriwa kutumia tund hili ili kujihakikishia ulinzi wa afya zao na wasisubiri mpaka wakutane nayo.

HUPUNGUZA SHINIKIZO LA DAMU KWA KIWANGO KIKUBWA.
 Utafiti uliofanywa na watu wamarekani ulibaini kuwa watu wengi walio na tatizo la shinikizo la damu (PRESURE) na wakatumia tunda hili katika milo yao waliweza kupunguza kasi ya tatizo hilo.
Hii inatokana na uwepo wa sukari asilia ambayo ni muhimu kurekebisha kiwango cha sukari mwilini na kukuleta kiwango sawa cha sukari inayohitajika.

MAGONJWA YA MENO NA MIFUPA. 
  Tikiti-maji lina madini kama vitamini C ambayo husaidia kuzuia magonjwa ya fizi pamoja na meno (KISEYEYE),hivyo ulaji wa tunda hili hasa kwa watoto utapunguza kasi ya athari za ugonjwa huu.
Watoto wengi pia hulipenda kutokana na sukari yake iliyomo ndani ya tunda hili hivyo haitakua vigumu mtoto kulila kwani kuna baadhi ya matunda ambayo sio rafiki kwa watoto na asilimia kubwa hayapendwi kutokana na uchachu,uchungu au kiwango kidogo cha sukari kinachopatikana.

HUIMARISHA UBONGO.
 Uwepo wa vitamini Bcomplex (B6) kwenye tunda hili husaidia kuimarisha kazi ya ubongo na kuufanya kuwa mchangamfu kwa muda mrefu.Baadhi ya matatizo yanayoyaukumba ubongo huweza kuzuiwa na kurekebishwa na vitamini hiyo.Unashauriwa kama wewe ni mwanafunzi utumie tunda hili kwa manufaa ya kuufanya ubongo wako kuwa active.Vilevile hata kwa wazee na walevi wanaokutana na matatizo ya kusahau watakuwa vizuri endapo watatumia tunda hili.Si kuimarisha tuu bali tunda hili hutumika kama lishe ya ubongo.


   Siyo ivyo tuu,licha ya kuchangia kwa kiasi kikubwa urekebishaji wa tatizo hilo tunda hili lina uwezo mkubwa sana wa kusaidia moyo kuweza kufanya kazi kwa kiwango sahihi na sio kuzidiwa na kazi.Hii husababisha kuupa moyo muda wa kutosha wa kupumzika kwa kufanya kazi kidogo.
  Unaweza aukatumia tunda hili kama juisi na pia ukala kama unavyokula matunda mengine ila vyote hufikisha virutubisho mwilini,lakini pia kwa matatizo mengine ambayo tumeyaona hapo juu unashauriwa kutengeneza juisi ya tunda hili bila kuondoa kitu chochote kile nikimaanisha kuanzia maganda mpaka mbegu zake.
      Anza mazoea sasa yakutumia matunda kama lishe mbadala na kinga dhidi ya magonjwa na usisubiri mpaka ukutane na magonjwa ndipo ukumbuke kuna lishe ya matunda,fanya hivyo kwa manufaa ya afya yako binafsi na sio kwa kulazimishwa wala kuiga ulaji wa mtu mwingne.
Ifahamike wazi kwamba ulaji wa matunda kiafya haukusababishii wewe usimwone daktari,bali kuna matatizo mengine ambayo ni lazima ukafanyiwe uchunguzi na ukatibiwe kwa mtaalamu wa afya kwani yanaweza kuwa ni zaidi ya ufikiriavyo.
 Kwa maoni,ushauri na mengineyo usisite kuwasiliana nasi kwa mawasiliano hapo chini. Ahsante

PHONE:  0673666791

Email: goldamplat@gmail.com