Ijumaa, 13 Januari 2017

EMBE
Uhali gani ndugu msomaji wa makala haya,ni matumaini yangu u mzima wa afya na mugu amekujalia kuamka salama hivyo tunapaswa kumshukuru kwa neema hii.Twende moja kwa moja kwenye mada yetu ya leo inayohusiana na tunda aina ya embe.


Katika matunda yenye sukari ni pamoja na tunda hili,ukiachilia mbali ndizi,nanasi na mapera.wengi wetu hupenda kulitumia tunda hili kama kutengenezea juisi,kulila likiwa limeiva au bichi na hata bidhaa za vindani kama vile achali na mango pickle.Wote huu ni ulaji ambao unaongeza virutubisho mwilini vilivyo katika embe.Faida nyingi huonekana katika ulaji wa embe na sio tuu nyama yake bali hata miziz,majani pamoja na maua yake pia,tuone baadhi.
MAGONJWA YA MACHO.
Embe lina vitamini A kwa kiwango kikubwa baada ya karoti ukilinganisha na matunda mengine,uwezo huu husaidia kudhibiti magonjwa ya ukavu macho na udhaifu mwingine wa macho.tumia embe kwa lengo la kutibu macho yako na sio kwa mazoea ya kula kwa kujifurahisha.

UDHAIFU WA TAYA NA MENO.
Uwepo wa vitamini C katika tunda hili,unahakikisha kazi ya uimarishaji wa meno na taya/fizi za meno.Kwani vitamini C huzuia ugonjwa wa udhaifu wa meno (scurvy).kula embe kawaida unaweza kulila likiwa lenyewe au ukatengeneza juisi ya tunda hili.

MALARIA SUGU.
Majani machanga ya mti wa muembe hutumika kama kinga na tiba ya malaria sugu kwa asilimia kubwa.Unaweza kuyatumia kwa kuyatafuna baada ya kuyaosha vizuri au pia unaweza kuyachemsha na kuyaacha yapoe kwa muda ndipo uyatumie maji na majani yenyewe.
NB: Katika kutibu ugonjwa huu hakikisha unakula majani haya machanga kwani yana nguvu kubwa ya kupambana na wadudu wa malaria sugu.

PUMU.
Majani ya muembe yakikaushwa vizuri katika kivuli (ili kuzuia alkadosisi kupotea) na kusagwa pia hutumika katika kutibu tatizo la pumu.Hii imewasaidia wengi katika kufanya ivyo na wameondokana na tatizo hilo.Saga majani hayo na uchanganye na maji kisha uyatumie kwa kunywa utapata matokeo.

MATATIZO YA UZAZI.
Tunda hili lina kokwa ambalo ndio dawa kubwa ya tatizo la kuziba mirija ya uzazi na tatizo hili haliwapati akina mama tuu bali hata kwa akina baba nao hukumbwa nalo.Chukua kokwa likaushe vizuri na ulisage ili kupata unga wake,halafu tumia unga huo kuchanganya na maji kisha kunywa hayo maji angalau glasi moja kabla ya mlo wako wowote ule.

Matatizo mengine kama ufinyu wa utoaji maziwa kwa akina mama wanaonyonyesha huondolewa kwa kutumia maua ya maembe,pia hata harufu mbaya ya mdomo huondolewa kwa matumizi ya majani ya maembe.
Utumiaji wa tunda hili kama dawa utaona mabadiliko yake ndani ya muda mfupi kama ukizingatia utaratibu wa lishe kiafya na sio kwa mzoea.
Nikushukuru kwa muda wako wa kusoma na nikuombe uanze kufanyia kazi kama kweli unataka mabadiliko kiafya na si uchukulie kawaida kama ulivyozoea.
Kwa ushauri,maoni na matatizo yoyote yahusuyo afya yako,usisite kuwasiliana nasi kwa;

Phone; 0673666791
Email; goldamplat@gmail.com amplat afya kwanza

Jumatano, 11 Januari 2017

 PAPAI


Habari za muda huu ndugu msomaji,naamini u mzima wa afya na furaha hivyo huna budi kumshukuru Mungu.Kwa wale walio na matatizo ya kiafya na kiakili nao hawana budi kumshukuru mungu kwani pumzi waliyopewa kwa siku ya leo inatosha kabisa kusema asante kwa Mungu wako.
   Leo tutaangalia umuhimu wa tunda la aina nyingine,ambalo ni papai.tunda hili pia sio geni na linafahamika na idadi kubwa ya watu nchini kwetu.Lichz ya kuwa watu wengine hula tunda hili kutokana na utamu wa sukari iliyomo ndani mwake,lakini ukweli kwamba tunda hili lina virutubisho vingi ambavyo vitakufafanya uwe na afya bora na uondokane na magonjwa mbalimbali,tuanze kuangalia tatizo moja baada ya lingine.

USAGAJI WA CHAKULA MWILINI.
 Watu wengi wanaopata choo kigumu ni wavivu wa kunywa maji,labda hawaoni umuhimu wake au wana mazoea ya kunywa maji pale wasikiapo kiu tuu.Utaratibu huu sio mzuri ingawa umezoeleka na watu wengi hivyio ni lazima tupingane nao.Kutokana na ulaini wa papai na kimeng"enya cha PAPAIN kilichopo ndani ya tunda hili,husaidia kulainisha chakula tumboni na kukifanya kiweze kusagika kwa urahisi zaidi.Ili uondokane na tatizo la usagaji wa chakula na magonjwa mengine yahusikayo na hayo,huna budi kutumia papai na kujizoesha kunywa maji mara nyingi uwezavyo kwa siku.Si tuu kwa ajili ya tatizo hili bali na matatizo mengine pia.


MAGONJWA YA UKOSEFU WA VITAMINI.
 Katika matunda yenye utajiri wa vitamini,papai ni mojawapo katika orodha kwani lina vitamini A,B,C,D na E.vitamini zote hizo hutumika kurekebisha magonjwa kama ukavu macho,kiseyeye na matege (kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 5).Vilevile magonjwa mengine ambayo sijayataja hapo juu yatokanayo na ukosefu wa vitamini hizo huzuiliiwa kwa kula papai kwani litasababisha uwepo wa vitamini hizo na kuzuia magonjwa hayo kutokea.

UPONYAJI WA VIDONDA.
 Ute ute/Maziwa ya papai hutumika kutibu vidonda vya aina zote,kuanzia vidonda vya ndani ya mwili hata vile vya nje ya mwili wa binadamu.Vidonda kama vya tumbo huweza kutibiwa kwa maziwa hayo yatokanayo na papai vile vile hata vidonda vya nje kama kuungua na kuumia sehemu fulani ya mwili hutibiwa kwa kupaka mafuta hayo sehemu iliyoathirika/yenye jeraha.
 

MAGONJWA YA INI NA FIGO.
 Ini ndio ogani pekee ambayo hupambana na sumu mwilini mwa binadamu,ukiachilia mbali figo ambayo kwa kiasi fulani huondoa sumu.Mbegu za papai hulipa ini nguvu za kuendelea kupambana na sumu ziingiazo mwilini mwetu na kukupunguzia kiwango kikubwa cha sumu ambazo zitaathiri afya yako.Pia majani ya mpapapi yakichemshwa kwa dakika 15 na kuutumiwa kwa kunywa angalau lita 1.5 kwa siku,husafisha kabisa figo na kuondoa matatizo yatokanayo na mfumo wa utoaji taka mwili (mfumo wa mkojo)

MAGONJWA YA MAPAFU.
  Kwa watumiaji wa sigara na wale wote wanaokumbana na adha za moshi kila kukicha,utumiaji wa papai utakupunguzia madhara ya moshi kwa asilimia kubwa (zaidi ya 80%).Kutokana na vitamini A iliyopo kwa wingi ndani ya tunda hili madhara yatokanayo na moshi huzuilika,kwani tunajua wazi kwamba moshi huathiri mfumo wa upumuaji wetu kwani ni hewa mbaya ambayo inaingia mwilini (kwenye mapafu) na kuingilia mfumo mzima wa upumuaji.
Wagonjwa wa macho pia nawashauri kutumia papai kama dawa na sio kama mlo wa mazoea tena,kwani kwa kufanya hivyo utajihakikishia usalama na uhai wa afya yako.
 Kwa ushauri na matatizo yanayohusu afya yako,wasiliana nasi muda wowote upate ushauri.Pia tunakaribisha maoni,mapendekezo na mitazamo mbalimbali.

Contact: 0673666791
Email: goldamplat@mail.com

Jumapili, 8 Januari 2017


       TANGO

Image result for faida za tango kiafyaImage result for faida za tango kiafya

Habari za tangu tulipokuwa pamoja muda uliopita,ni matumaini yangu ni wazima wa afya na hatuna budi kumshukuru mwanyezi mungu.Kwa wale walio wagonjwa na hawajiwezi mungu awasaidie na niwape pole pia.
Tuanze na mada yetu muhimu ya kutambua umuhimu wa virutubisho vipatikanavyo ndani ya matunda.Tuanze na umuhimu wa Tango,kama tunavyolifahamu tunda hili ni muhimu kwa afya kwani lina kazi nyingi sana katika miili yetu.maganda yake na mbegu zake ndio huwa na umuhimu mkubwa kama tutakavyoona.




Tunapoongelea umuhimu wa tango tunaona uwezo wake mkubwa katika kutibu na kuzuia magonjwa mbalimbali kama vile;

MAGONJWA YA NGOZI.
Tango hujulikana kwa kuwa na maji mengi ambayo husaidia kulainisha ngozi,tangu zamani tunda hili lilitumika katika kutibu magonjwa ya ngozi.Weusi upatikanao kuzunguka maeneo ya macho,huweza kuondolewa kwa kutumia vipande kadhaa vya tango.Chukua vipande viwili vya tango na usugulie kuzunguka eneo lenye weusi,kwa kufanya hivyo utaweza kutibu eneo hilo.

HARUFU MBAYA MDOMONI.
Kama kinywa chako kinatoa harufu mbaya na unashindwa kuzuia,unaruhusiwa kutumia kipande kimoja hadi viwili kwa kutafuna.Kwa kufanya hivyo utazuia harufu mbaya mdomoni.

KUONGEZA UTE KWENE JOINTI.
Ifahamike kwamba maji yapatikanayo kwenye tango husaidia pia katika kuongeza uteute katika joint za mwilini.Hii huzuia mifupa kusagana na hivyo matatizo ya mifupa kushughulikiwa ipasavyo.kula tango kwa lengo la kutibu matatizo na sio kwa mazoea.

  Faida nyingine za tango ni kama vile,kusafisha kiatu cha rangi nyeusi na kufanya king"ae zaidi.Tango lina vitamini B1,B2,B3,B4,B6 na B12 pia lina kashiumu na potashium kwa wingi.