Jumatano, 11 Januari 2017

 PAPAI


Habari za muda huu ndugu msomaji,naamini u mzima wa afya na furaha hivyo huna budi kumshukuru Mungu.Kwa wale walio na matatizo ya kiafya na kiakili nao hawana budi kumshukuru mungu kwani pumzi waliyopewa kwa siku ya leo inatosha kabisa kusema asante kwa Mungu wako.
   Leo tutaangalia umuhimu wa tunda la aina nyingine,ambalo ni papai.tunda hili pia sio geni na linafahamika na idadi kubwa ya watu nchini kwetu.Lichz ya kuwa watu wengine hula tunda hili kutokana na utamu wa sukari iliyomo ndani mwake,lakini ukweli kwamba tunda hili lina virutubisho vingi ambavyo vitakufafanya uwe na afya bora na uondokane na magonjwa mbalimbali,tuanze kuangalia tatizo moja baada ya lingine.

USAGAJI WA CHAKULA MWILINI.
 Watu wengi wanaopata choo kigumu ni wavivu wa kunywa maji,labda hawaoni umuhimu wake au wana mazoea ya kunywa maji pale wasikiapo kiu tuu.Utaratibu huu sio mzuri ingawa umezoeleka na watu wengi hivyio ni lazima tupingane nao.Kutokana na ulaini wa papai na kimeng"enya cha PAPAIN kilichopo ndani ya tunda hili,husaidia kulainisha chakula tumboni na kukifanya kiweze kusagika kwa urahisi zaidi.Ili uondokane na tatizo la usagaji wa chakula na magonjwa mengine yahusikayo na hayo,huna budi kutumia papai na kujizoesha kunywa maji mara nyingi uwezavyo kwa siku.Si tuu kwa ajili ya tatizo hili bali na matatizo mengine pia.


MAGONJWA YA UKOSEFU WA VITAMINI.
 Katika matunda yenye utajiri wa vitamini,papai ni mojawapo katika orodha kwani lina vitamini A,B,C,D na E.vitamini zote hizo hutumika kurekebisha magonjwa kama ukavu macho,kiseyeye na matege (kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 5).Vilevile magonjwa mengine ambayo sijayataja hapo juu yatokanayo na ukosefu wa vitamini hizo huzuiliiwa kwa kula papai kwani litasababisha uwepo wa vitamini hizo na kuzuia magonjwa hayo kutokea.

UPONYAJI WA VIDONDA.
 Ute ute/Maziwa ya papai hutumika kutibu vidonda vya aina zote,kuanzia vidonda vya ndani ya mwili hata vile vya nje ya mwili wa binadamu.Vidonda kama vya tumbo huweza kutibiwa kwa maziwa hayo yatokanayo na papai vile vile hata vidonda vya nje kama kuungua na kuumia sehemu fulani ya mwili hutibiwa kwa kupaka mafuta hayo sehemu iliyoathirika/yenye jeraha.
 

MAGONJWA YA INI NA FIGO.
 Ini ndio ogani pekee ambayo hupambana na sumu mwilini mwa binadamu,ukiachilia mbali figo ambayo kwa kiasi fulani huondoa sumu.Mbegu za papai hulipa ini nguvu za kuendelea kupambana na sumu ziingiazo mwilini mwetu na kukupunguzia kiwango kikubwa cha sumu ambazo zitaathiri afya yako.Pia majani ya mpapapi yakichemshwa kwa dakika 15 na kuutumiwa kwa kunywa angalau lita 1.5 kwa siku,husafisha kabisa figo na kuondoa matatizo yatokanayo na mfumo wa utoaji taka mwili (mfumo wa mkojo)

MAGONJWA YA MAPAFU.
  Kwa watumiaji wa sigara na wale wote wanaokumbana na adha za moshi kila kukicha,utumiaji wa papai utakupunguzia madhara ya moshi kwa asilimia kubwa (zaidi ya 80%).Kutokana na vitamini A iliyopo kwa wingi ndani ya tunda hili madhara yatokanayo na moshi huzuilika,kwani tunajua wazi kwamba moshi huathiri mfumo wa upumuaji wetu kwani ni hewa mbaya ambayo inaingia mwilini (kwenye mapafu) na kuingilia mfumo mzima wa upumuaji.
Wagonjwa wa macho pia nawashauri kutumia papai kama dawa na sio kama mlo wa mazoea tena,kwani kwa kufanya hivyo utajihakikishia usalama na uhai wa afya yako.
 Kwa ushauri na matatizo yanayohusu afya yako,wasiliana nasi muda wowote upate ushauri.Pia tunakaribisha maoni,mapendekezo na mitazamo mbalimbali.

Contact: 0673666791
Email: goldamplat@mail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni