Ijumaa, 13 Januari 2017

EMBE
Uhali gani ndugu msomaji wa makala haya,ni matumaini yangu u mzima wa afya na mugu amekujalia kuamka salama hivyo tunapaswa kumshukuru kwa neema hii.Twende moja kwa moja kwenye mada yetu ya leo inayohusiana na tunda aina ya embe.


Katika matunda yenye sukari ni pamoja na tunda hili,ukiachilia mbali ndizi,nanasi na mapera.wengi wetu hupenda kulitumia tunda hili kama kutengenezea juisi,kulila likiwa limeiva au bichi na hata bidhaa za vindani kama vile achali na mango pickle.Wote huu ni ulaji ambao unaongeza virutubisho mwilini vilivyo katika embe.Faida nyingi huonekana katika ulaji wa embe na sio tuu nyama yake bali hata miziz,majani pamoja na maua yake pia,tuone baadhi.
MAGONJWA YA MACHO.
Embe lina vitamini A kwa kiwango kikubwa baada ya karoti ukilinganisha na matunda mengine,uwezo huu husaidia kudhibiti magonjwa ya ukavu macho na udhaifu mwingine wa macho.tumia embe kwa lengo la kutibu macho yako na sio kwa mazoea ya kula kwa kujifurahisha.

UDHAIFU WA TAYA NA MENO.
Uwepo wa vitamini C katika tunda hili,unahakikisha kazi ya uimarishaji wa meno na taya/fizi za meno.Kwani vitamini C huzuia ugonjwa wa udhaifu wa meno (scurvy).kula embe kawaida unaweza kulila likiwa lenyewe au ukatengeneza juisi ya tunda hili.

MALARIA SUGU.
Majani machanga ya mti wa muembe hutumika kama kinga na tiba ya malaria sugu kwa asilimia kubwa.Unaweza kuyatumia kwa kuyatafuna baada ya kuyaosha vizuri au pia unaweza kuyachemsha na kuyaacha yapoe kwa muda ndipo uyatumie maji na majani yenyewe.
NB: Katika kutibu ugonjwa huu hakikisha unakula majani haya machanga kwani yana nguvu kubwa ya kupambana na wadudu wa malaria sugu.

PUMU.
Majani ya muembe yakikaushwa vizuri katika kivuli (ili kuzuia alkadosisi kupotea) na kusagwa pia hutumika katika kutibu tatizo la pumu.Hii imewasaidia wengi katika kufanya ivyo na wameondokana na tatizo hilo.Saga majani hayo na uchanganye na maji kisha uyatumie kwa kunywa utapata matokeo.

MATATIZO YA UZAZI.
Tunda hili lina kokwa ambalo ndio dawa kubwa ya tatizo la kuziba mirija ya uzazi na tatizo hili haliwapati akina mama tuu bali hata kwa akina baba nao hukumbwa nalo.Chukua kokwa likaushe vizuri na ulisage ili kupata unga wake,halafu tumia unga huo kuchanganya na maji kisha kunywa hayo maji angalau glasi moja kabla ya mlo wako wowote ule.

Matatizo mengine kama ufinyu wa utoaji maziwa kwa akina mama wanaonyonyesha huondolewa kwa kutumia maua ya maembe,pia hata harufu mbaya ya mdomo huondolewa kwa matumizi ya majani ya maembe.
Utumiaji wa tunda hili kama dawa utaona mabadiliko yake ndani ya muda mfupi kama ukizingatia utaratibu wa lishe kiafya na sio kwa mzoea.
Nikushukuru kwa muda wako wa kusoma na nikuombe uanze kufanyia kazi kama kweli unataka mabadiliko kiafya na si uchukulie kawaida kama ulivyozoea.
Kwa ushauri,maoni na matatizo yoyote yahusuyo afya yako,usisite kuwasiliana nasi kwa;

Phone; 0673666791
Email; goldamplat@gmail.com amplat afya kwanza

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni