TANGO
Habari za tangu tulipokuwa pamoja muda uliopita,ni matumaini yangu ni wazima wa afya na hatuna budi kumshukuru mwanyezi mungu.Kwa wale walio wagonjwa na hawajiwezi mungu awasaidie na niwape pole pia.
MAGONJWA YA NGOZI.
Tango hujulikana kwa kuwa na maji mengi ambayo husaidia kulainisha ngozi,tangu zamani tunda hili lilitumika katika kutibu magonjwa ya ngozi.Weusi upatikanao kuzunguka maeneo ya macho,huweza kuondolewa kwa kutumia vipande kadhaa vya tango.Chukua vipande viwili vya tango na usugulie kuzunguka eneo lenye weusi,kwa kufanya hivyo utaweza kutibu eneo hilo.
HARUFU MBAYA MDOMONI.
Kama kinywa chako kinatoa harufu mbaya na unashindwa kuzuia,unaruhusiwa kutumia kipande kimoja hadi viwili kwa kutafuna.Kwa kufanya hivyo utazuia harufu mbaya mdomoni.
KUONGEZA UTE KWENE JOINTI.
Ifahamike kwamba maji yapatikanayo kwenye tango husaidia pia katika kuongeza uteute katika joint za mwilini.Hii huzuia mifupa kusagana na hivyo matatizo ya mifupa kushughulikiwa ipasavyo.kula tango kwa lengo la kutibu matatizo na sio kwa mazoea.
Faida nyingine za tango ni kama vile,kusafisha kiatu cha rangi nyeusi na kufanya king"ae zaidi.Tango lina vitamini B1,B2,B3,B4,B6 na B12 pia lina kashiumu na potashium kwa wingi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni